Rais Kikwete ahudhuria kikao cha SADC jijini CAPE TOWN

Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya SADC Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete(Watatu kushoto) akiongoza kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya SADC kilichofanyika jijini Cape Town Afrika ya Kusini leo.Wengine katika picha ni wajumbe wa kamati hiyo akiwemo mwenyeji Rais Jackob Zuma wa Afrika ya Kusini(kulia),Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Namibia Bibi Netumbo Nandi-Ndaitwa(kushoto) na wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa SADC Dkt.Tomaz Salomao.
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akijadiliana jambo na Katibu mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Dkt.Tomaz Salomao mjini Cape Town Afrika ya Kusini leo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mwenyeji wake Rais Jackob Zuma wa Afrika ya Kusini wakitoka katika ukumbi wa hoteli ya Westin jijini Cape Town Afrika ya Kusini mara baada ya kumalizika kwa kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalma ya SADc kilichofanyika leo.Rais Kikwete alikuwa nchini Afrika ya Kusini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mkurugenzi Mtendaji na mratibu wa asasi ya Bill and Melinda Gates Foundation Bwana Mark Suzman jijini Cape Town Afrika ya Kusini.Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo Adam Malima.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagana na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Misaada la Marekani USAID Dkt. Rajiv Shah muda mfupi baada ya kufanya naye mazungumzo katika ukumbi wa Cape Town Convention Centre jana.Picha na Freddy Maro.

Rais Kikwete awasili nchini Afrika Kusini kuhudhilia kikao cha viongozi Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Cape Town, Afrika ya Kusini kuhudhuria kikao cha viongozi Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachofanyika leo tarehe 10 Mei, 2013.
 
Viongozi wa SADC wanakutana chini ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ambayo Tanzania ndiye mwenyekiti. 

 
Kikao cha leo kinatarajia kuzungumzia maendeleo na hali ya usalama katika ukanda huu hususan hali ya usalama Mashariki mwa Kongo, DRC, Madagascar na Zimbabwe.
 
Nchi za Afrika ya Kusini, Malawi na Tanzania zitapeleka vikosi Mashariki mwa DRC kulinda na kuleta utulivu na usalama. 

 
Kuhusu Madagascar, nchi hiyo inatarajia kufanya uchaguzi Julai, 2013 wakati nchini Zimbabwe nako uchaguzi unatarajiwa kufanyika baadae mwaka huu. 

 
Mbali na mkutano huo Rais anahudhuria mikutano kadhaa inayoendelea mjini Capetown ukiwemo ule wa Kiuchumi ambao viongozi wa kisiasa, kiserikali na wakubwa wa mashirika binafsi wanahudhuria na kuzungumzia fursa za kibiashara na kiuchumi barani Afrika. 

 
Rais anatarajia kurejea Dar es Salaam kesho tarehe 11 Mei, 2013
 
“Mwisho”
 
Imetolewa na:
Premi Kibanga
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Cape Town – Afrika ya Kusini
10 Mei, 2013

RAIS KIKWETE AANZA ZIARA RASMI YA SIKU MBILI NCHINI KUWAIT LEO

k1Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mtawala wa Dola ya Kuwait Amiri Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kuwait City leo Mei 5, 2013 tayari kuanza ziara rasmi ya siku mbili katika nchi hiyo.

k2Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mtawala wa Dola ya Kuwait Amiri Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah wakipokea mashada ya mauwa alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kuwait City leo Mei 5, 2013 tayari kuanza ziara rasmi ya siku mbili katika nchi hiyo.k3k4k5

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mtawala wa Dola ya Kuwait Amiri Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah wakiingia sehemu ya mapokezi na kukagua gwaride rasmi mara tu alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kuwait City leo Mei 5, 2013 tayari kuanza ziara rasmi ya siku mbili katika nchi hiyo.k6k7

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mtawala wa Dola ya Kuwait Amiri Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah katika mazungumzo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kuwait City leo Mei 5, 2013 tayari kuanza ziara rasmi ya siku mbili katika nchi hiyo.PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE AMLAKI WAZIRI MKUU WA DENMARK ANAYETEMBELEA TANZANIA LEO


 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt muda mfupi baaday kuwasili katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jioni hii
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt wakipokea heshima za nyimbo za Taifa pamoja na saluti ya mizinga 21  katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akikagua gwaride lililoandaliwa kwa heshima yake
 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt na mwenyeji wake wakifurahia burudani mbalimbali
 Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akipkea shada l maua
Waziri mkuu wa Denmark Mhe.Helle Thorning-Schmidt akisalimiana na kinamama waliofurika uwanjani kumlaki. Picha na Freddy Maro

RAIS KIKWETE ASHIRIKI UTIAJI SAINI MPANGO WA UMOJA WA MATAIFA WA AMANI, USALAMA NA USHIRIKIANO KATIKA DRC

 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013.

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika  Dkt Nkosazana Clarice Dlamini-Zuma akisaini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013.
Rais Joseph Kabila wa DRC na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakibadilishana mawazo kwa furaha huku Rais wa Jamhuri ya Kongo (Brazaville) Mhe Denis Sassou Nguesso akiwa kati yao baada ya wote kweka saini katika Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 4, 2013.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe Ban Ki-moon akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maal: umu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Mahadhi Juma Maalim na wajumbe wengine wa ujumbe wa Tanzania wakati wa uwekaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 4, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe. Hailemariam Desalegn baada uwekaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 4, 2013. Katikati ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa Dkt Nkosazana Clarice Dlamini-Zuma.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon kwa kuwa mmoja wa viongozi wa bara la Afrika walio mstari wa mbele kusimamia amani baada uwekaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 4, 2013.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe Ban Ki-moon katika picha ya pamoja na viongozi wa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu baada ya uwekaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 4, 2013.PICHA NA IKULU

Rais Kikwete katika mkutano wa SADC nchini Msumbiji

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji wakiwa katika mkutano wa wakuu wa ncho za Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika SADC jijini Maputo Msumbiji jana.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) na Mwenyeji Rais Armando Guebuza wa Msumbiji wakati wa kikao cha SADC jijini Maputo jana(picha na Freddy Maro).

Rais Kikwete awasili Maputoleo kuhudhuria mkutano wa SADC

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya nchi jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la heshima muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo.Rais Kikwete yupo nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za SADC.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mwenyeji wake Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji katika ikulu ya jijini Maputo leo.Rais Kikwete yupo nchini Msumbiji kuhudhuria kikao cha viongozi wa jumuiya ya uchumi kusini mwa Afrika SADC
 Akisindikizwa na mwenyeji wake
Akiagana na mwenyeji wake

Rais Kikwete ahudhuria Mkutano wa AU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa ufafanuzi kuhusu hoja mbalimbali zilizoibuliwa na jopo la APRM kuhusu Demokrasia na Utawala Bora nchini Tanzania. Mhe. Rais alitoa ufafanuzi huo mbele ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Mhe. Jacob Zuma, Rais wa Afrika Kusini na Mhe. Paul Kagame, Rais wa Rwanda nao walihudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa AU ambapo Tanzania iliwasilisha ripoti yake kuhusu Demokrasia na Utawala Bora.
Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea kutoa ufafanuzi kuhusu masuala ya Demokrasia na Utawala Bora nchini Tanzania. Wengine katika picha ni Waziri Bernard K. Membe (Mb) (wa pili kulia), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakiwemo pia wajumbe na Wabunge waliofuatana na Mhe. Rais Kikwete kuhudhuria Mkutano huo.
Mhe. Rais Kikwete (kushoto) akibadilishana mawazo na Mhe. Salum Barwany, Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini nje ya ukumbi wa mkutano nchini Ethiopia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete katika picha ya pamoja na ujumbe aliofuatana nao nchini Ethiopia ambao unajumuisha Mawaziri, Wabunge na Timu ya APRM, Tanzania. 

Picha na  Ally Kondo, Addis Ababa

PRESIDENT KIKWETE AT WORLD ECONOMIC FORUM 2013 IN DAVOS


 President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets Belgium Princess Astrid in Davos Switzerland during the World Economic forum. The two leaders later participated in a Global Health and Diplomacy Dinner.
 President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with Global Fund Executive Director Dr.Mark Dybul(second left) at Hotel Sheraton in Davos Switzerland during the World Economic forum. Left is  Global Fund’s Director for Resource Mobilization Dr.Christoph Benn.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete speaks with Germany Federal Minister for Development Mr. Dirk Niebel  at Hotel Sheraton in Davos During the World Economic Forum(WEF) meeting yesterday.

President Kikwete and Tony Blair attend meeting on Mobilising Private Sector investment in African Energy

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete (right) speaks during a World Economic Forum session on “Mobilizing Private Sector Investment in African Energy,” held at World Food Programme Tent in Davos, Switzerland. On the left is USAID administrator Dr. Rajiv Shah and second left is former British Prime Minister Tony Blair.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and former British Prime Minister Tony Blair leaves World Food Programme tent in Davos, Switzerland after participating in a meeting on “Mobilizing Private Sector Investment in African energy,” yesterday
Photos by Freddy Maro

President Kikwete visits FIFA headquarters in Zurich.Meets FIFA President SEPP Blatter

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete bids farewell to his host FIFA president Joseph Sepp Blatter after visiting FIFA headquarters in Zurich, Switzerland at the invitation of Mr. Blatter
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete with FIFA President Joseph Sepp Blatter at FIFA headquarters in Zurich.
FIFA president Joseph Sepp Blatter shows President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete various World trophies on display at FIFA headquarters in Zurich, Switzerland.

Mama Salma Kikwete Atembelea Foundation Pour na AMREF Nchini Ufaransa


Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mwanzilishi na Rais wa Foundation Pour  l¨ Enfrance Mama Anne Aymone Giscard d’ Estaing na Mke wa Rais Mstaafu wa Ufaransa Bwana Valery Giscard d’ Estaing, wakati Mama Salma alipotembelea makao makuu ya taasisi hiyo jijini Paris Ufaransa tarehe 22:1:2013: Mama Salma yupo nchini Ufaransa akifuatana na Rais Kikwete kwenye ziara ya kiserikali nchini humo:
Rais wa AMREF France Bwana Nicolas Merindol akimkaribisha Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete kwenye makao makuu ya shirika hilo jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 22, 1, 2013 na baadaye viongozi hao walifanya mazungumzo juu ya ushirikiano zaidi wa taasisi hizo katika masuala ya afya na elimu

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA NCHINI UFARANSA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Rais wa Seneti ya Ufaransa Mhe. Jean Pierre Bel, alipotembelea makao makuu yake jijini Paris.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa zawadi kwa Rais wa Seneti ya Ufaransa Mhe. Jean Pierre Bel, alipotembelea makao makuu yake jijini Paris.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akiongea na Rais Mstaafu wa Ufaransa Mhe Valery Giscard d’Estaing na ujumbe wake katika hafla ya chakula cha usiku alichoandaa Rais huyo Mstaafu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tanzania Wildlife Foundation jijini Paris.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Kiongozi wa jumuiya ya Ismailia duniani,HH The Aga Khan alipomtembelea kwenye Hotel ya le Meurice jijini Paris.

PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE APOKELEWA RASMI NCHINI UFARANSA NA RAIS FRANCOIS HOLLANDE

 

  Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima
yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi
kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini humo
 Gari
iliyomchukua Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikiondoka Ikulu ya nchi hiyo
maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo
Januari 21, 2013.
  Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima
yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi
kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini humo
  Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais Francois Hollande
wa Ufaransa katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee
(hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013.
 
 Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akiwa katika maongezi rasmi na
mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa na ujumbe wake  katika
Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee)
jijini Paris leo Januari 21, 2013.
 
  Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na mwenyeji wake Rais Francois
Hollande wa Ufaransa baada ya mazungumzo yao rasmi katika Ikulu ya nchi
hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris
leo Januari 21, 2013

 

Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa
Ufaransa wakiongea na wanahabari baada ya mazungumzo yao rasmi katika
Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee)
jijini Paris leo Januari 21, 2013.PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA KIKWETE WAWASILI NCHINI UFARANSA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mke wa Rais wa Mali,Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na mke wa Rais wa Mali,Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu nchini humo.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Begum Taj na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mhe. Marcel Escure
wakimsubiri Rais Jakaya Kikwete uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, tayari kuanza ziara ya yake ya kiserikali ya siku tatu.
Mama Salma Kikwete akionega na mke wa Rais wa Mali,Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE A REJEA NCHINI BAADA YA KUHUDHURIA KIKAO CHA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI NAIROBI, KENYA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakishuhudia utiwaji saini mkataba wa haja ya kuwepo kwa ushirikiano wa kibiashara kati ya Marekani na nchi za Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Zoezi hili lilifanywa baina ya Mawaziri wa Bishara wa nchi wanachama wa Jumuiya na Kaimu Waziri wa Bishara wa Marekani Bi Rebecca Blank aliyehudhuria kikao hicho.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia Rais Mwai Kibaki wa Kenya akimkabidhi nyundo Rais Yoweri Muzeveni kama ishara ya kukabidhi Uienyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wenzie wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa nne wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi,
Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza kijana Joel Adagson Mwigomole kwa kuibuka mshindi wa pili wa kuandika Insha kwa wanafunzi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa mkutano wa nne wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya. Joel ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mzumbe, Morogoro.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Yoweri Museveni wa Uganda akimpongeza kijana Joel Adagson Mwigomole kwa kuibuka mshindi wa pili wa kuandika Insha kwa wanafunzi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa mkutano wa nne wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.Joel ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mzumbe, Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wenzie wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na washiriki mwishoni mwa kikao cha nne cha Jumuiya nje ya Jengo la Mikutano wa Kimataifa la Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagwa kwa heshima wakati anaondoka jijini Nairobi, Kenya.PICHA NA IKULU.

RAIS KIKWETE NA VIONGOZI WENZIE WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA BARABARA YA ARUSHA-NAMANGA-ATHI RIVER

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012 tayari kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012 tayari kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu.Kulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Kenya,Mh. Batilda – Salha Burhan.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kushoto) akiwa katika mazungumzo na Kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ismailia Mtukufu Aga Khan (kushoto) katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012.Rais Kikwete yupo nchini Kenya kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu.Wengine Pichani ni Rais wa Kenya,Mh. Mwai Kibaki (katikati) na Rais wa Burundi,Mh. Nkurunzinzah.
Wakati wa Wimbo wa Taifa.
Baadhi ya mawaziri na makatibu wakuu wa Tanzania waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania.
Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la nchini Kenya wakiwa kwenye Sherehe hiyo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia kwenye sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakipata maelezo ya Barabara hiyo itakavyokuwa kutoka kwa Injinia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikata utepe kwa pamoja kuzindua rasmi wa Barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali waliofanikisha ujenzi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River.PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE AREJEA NCHINI LEO

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara alipowasili kutoka katika ziara rasmi ya siku nne nchini Oman.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi waliojitokeza kumpokea leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara alipowasili kutoka katika ziara rasmi ya siku nne nchini Oman.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam Suleiman Kova leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara alipowasili kutoka katika ziara rasmi ya siku nne nchini Oman.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Jordan Rugimbana leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara alipowasili kutoka katika ziara rasmi ya siku nne nchini Oman.

Rais Kikwete aweka jiwe la Msingi kuzindua ujenzi wa Jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Oman

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania  nchini Oman katika mtaa wa balozi jijini Muscat Oman jana.Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe, (watatu kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Oman, Ali Ahmed Saleh na (kulia) ni Afisa Mwandamizi Ubalozi wa Tanzania nchini Oman,  Bwana Abdallah Kilima.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizindua ujenzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini Oman jana.Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe,watatu kushoto ni  Balozi wa Tanzania nchini Oman, Bw. Ali Ahmed Saleh, (wanne kulia aliyeshika karai) ni Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Oman, Bw. Abdallah Kilima na (kulia anayeshuhudia) ni  Afisa katika Ubalozi huo, Bw. Saidi Mussa.Picha na Freddy Maro-IKULU


Serikali ya kifalme ya Oman inatarajia kutuma ujumbe wake ambao utajumuisha na   wafanyabiashara kuja Tanzania  kutathmini na kuangalia maeneo gani nchi hiyo na wafanyabiashara wake wanaweza kuwekeza ,kufuatia ziara ya kiserikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete  ya siku 4 nchini Oman.
“Tutaunda kamati na kutuma ujumbe kwenda Tanzania kuangalia na kujua  aina gani ya biashara na vitega uchumi Oman inaweza kuwekeza”.AmesemaNaibu Waziri Mkuu wa serikali ya kifalme ya Oman, Mheshimiwa Sayyid Fahad Mahmood Al Said wakati wa mazungumzo yao ya kiserikali.
Naibu Waziri Mkuu huyo amesema Oman ina matumaini makubwa kuhusu mazungumzo yao ya tarehe 17
Octoba, 2012 yaliyofanyika katika makao makuu ya Baraza la Mawaziri.
Amesema Baraza la Mawaziri la nchi yake litakaa na kujadiliana pamoja na Chama cha wafanyibiashara na Viwanda kuandaa serikali ya kuja Tanzania na kuhakimisha mahusiano yetu yanadumu.
Rais amemueleza Makamu wa Waziri Mkuu kuwa Tanzania hivi karibuni imegundua gesi kwa wingi na hivyo kuna changamoto kubwa ya kujenga uwezo kwa watu wake waweze kujadiliana na kuwekeana mikataba itakayoleta tija kwa Taifa na watu wake.
Rais Kikwete pia amekutana na watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchini Oman ambapo amewaeleza kwa kifupi maendeleo yanayoletwa na serikali katika Nyanja za Kilimo, Elimu, Afya, miundombinu na mambo mbalimbali ya kisiasa yanayoendelea nchini Tanzania.
Watanzania hao, nao wamepata nafasi ya kuelezea matatizo na matarajio yao kwa Rais , ambapo Rais amewapata nafasi ya kufafanua na kujibu baadhi ya hoja zao na kuwapa changamoto watanzania wote wanaoishi nchi za nje  ya kushiriki katika shughuli za  maendeleo na  kukuza Uchumi wa Tanzania kwa kutafuta na kushawishi wawekezaji na marafiki mbalimbali kusaidia katika nyanja mbalimbali ambazo zinahitaji misaada ya maendeleo.

Rais anamaliza ziara yake tarehe 18 Octoba, 2012 na kurejea nyumbani jioni.




Tanzania and Oman signed various agreements aimed at enhancing political and economic ties between the two countries

Tanzania and The Sultanate of Oman yesterday signed various agreements aimed at enhancing political and economic ties between the two countries. 
The Agreements were signed during the second day of President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete’s State Visit to the Sultanate following the invitation of His Majesty Sultan Qaboos bin Said Al Said. 
The agreements were signed yesterday during the joint Tanzania- Oman business forum held at AL Bustan Hotel in Muscat Oman including, The Agreement on Promotion and Protection of Investment, Memorandum of Understanding on Cooperation in higher Education between Oman and Zanzibar, Agreement on Cooperation in Records and Archives and the Agreement on Forming joint Business Council between Oman and Tanzania. In the Pictures below;
The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation Bernard Membe and Oman Ministry of Financial Affairs Secretary General, Sultan bin Salim Al Habsi sign and exchange legal instruments on the Agreement on Promotion and Protection of Investment.Witnessing the signing in President Dr.Jakaya Kikwete.
Zanzibar’s Minister for Labour, Cooperatives and Economic Empowerment, Haroun Ali Suleiman and Oman Minister for Higher Education Dr. Rawiyah AL Busaidi sign and exchange legal instruments on Memorandum of Understanding on Cooperation in higher Education between Oman and Zanzibar while President Dr.Jakaya Kikwete witness the signing ceremony.
The Permanent Secretary ,President’s Office(Civil Service) Mr. George Yambesi and Oman’s Ministry of Heritage and Culture under Secretary,Dr.Hamed bin Mohamed AL Dhawyan sign and exchange legal instruments on Agreement on Cooperation in Records and Archives.
The President of Tanzania chamber of Commerce, Agriculture and Industry Mr.Aloyce joseph Mwamanga and Oman’s President of Chamber of Commerce and Industry Mr.Khalil Abdullah Al konji sing an Agreement on Forming joint Business Council between Tanzania and Oman(photos by Freddy Maro).

Rais Kikwete aongoza mkutano wa Wafanyabishara wa Oman na Tanzania jijini Muscat

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wafanyabiashara wa Oman na Tanzania wakati wa mkutano malum wa uwekezaji aliouandaa kwaajili ya kuelezea fursa za uwekezaji nchini.Mkutano huo wa uwekezaji ulofanyika jijini Muscat Oman ulihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe,Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Abdallah Kigoda ,Wziri wa Kazi,Ushirika na Uwezeshaji kiuchumi wa  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haroun Ali Suleiman pamoja na Naibu Waziri wa Fedha Janet Mbene.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya Wafanyabishara wa Oman na Tanzania waliohudhuria mkutano maalum wa uwekezaji Tanzania ulifanyika jijini Muscat Oman leo .Mkutano huo wa uwekezaji ulofanyika jijini Muscat Oman ulihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe,Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Abdallah Kigoda ,Wziri wa Kazi,Ushirika na Uwezeshaji kiuchumi wa  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haroun Ali Suleiman pamoja na Naibu Waziri wa Fedha Janet Mbene.Pamoja na viongozi waandamizi  wa serikali zote mbili.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mawaziri na maofika wangazi za juu wa Oman na Tanzania waliohudhuria mkutano maalum wa uwekezaji uliofanyika katika Hoteli ya Al Bustan jijini Muscat Oman leo. Picha na Freddy Maro
******************************************************
******************************************************

H.E. Khalil Al Khonji, Chairman, Oman Chamber of Commerce and Industry;

Eng. Aloys J. Mwamanga, President, Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture;

Ms. Munira Humoud Said, President, Zanzibar Chamber of Commerce, Industry and Agriculture;

Honorable Ministers;

Distinguished Businessmen and Women;

Invited Guests;

Ladies and Gentlemen;

I thank you Mr. Khalil Al Khonji, Chairman of the Oman Chamber of Commerce and Industry for inviting me to attend and speak at the historic first, Tanzania – Oman Business Forum. I thank the Oman Chamber of Commerce and Industry and the Tanzania Embassy for conceiving the idea of holding this important meeting and organizing it so well. I am visiting the Sultanate of Oman, at the invitation of His Majesty Sultan Qaboos, to consolidate the longstanding historic social, political and economic relations and cooperation that so happily exists between our two countries and peoples. This, Forum, therefore is a vehicle for promoting and strengthening economic, trading and investment cooperation between our governments and peoples. I wish events of this nature could take place more often and regularly, both here in Oman and back home in Tanzania.

Ladies and Gentlemen;

The Sultanate of Oman is a very special country to Tanzania. There is no other country on this planet with as many of its citizens who have blood relations with the people of Tanzania. This is a unique asset or resource which our two countries can use to promote stronger political, social and economic ties for the mutual benefit of our two countries and two peoples. I am undertaking this visit and I speak at this Forum this afternoon precisely for that reason.

Ladies and Gentlemen;

I heartily welcome the holding of this Forum and I look forward with great anticipation to the outcome of this meeting. I hope Oman and Tanzanian business people and the several government officials gathered here this afternoon will rise to the occasion and take our economic relations to the next level. I want to see increased economic, investment and business relations between our two friendly countries become more robust because we both have a lot to offer to each other and much to benefit.

Ladies and Gentlemen;

Let me start by stating emphatically that Tanzania is a great place to invest and do business. We have worked so hard for over two decades now to put in place a very conducive investment environment. We have opened our doors wide for anyone interested to bring capital and do business with us. We offer a wide range of investment incentives just like several other popular investment destinations in the world. And, in some respect we are even more generous and attractive.

I am happy that I have brought with me responsible government officials and some businessmen from both Zanzibar and Tanzania Mainland who will give you detailed information and answer all your questions.

Peace, Good Governance and Conducive Business Environment

Ladies and Gentlemen;

Tanzania is a peaceful and politically stable country. This is a critical asset for one to invest. We are a young vibrant multiparty democracy. We uphold the tenets of good governance, respect of human rights and the rule of law. The fight against corruption and other vices in society is unwavering, despite the daunting challenges we are faced with.

Private investments in Tanzania are guaranteed by government policy and law against nationalization and expropriation. Investors are allowed to take their money. They can repatriate profits and dividends without inhibitions. Besides, Tanzania is a signatory and a party to several multilateral and bilateral agreements on protection and promotion of investments. Among such international agreements and memberships, Tanzania is a member of Multilateral Investment Guarantee Agency of the World Bank (MIGA) and the Swiss based International Centre for Settlement of Investment Disputes (ICSID).

At the bilateral level, Tanzania has entered into investment promotion and protection agreements with many countries. I am happy that, shortly before my coming here we witnessed the signing of the Agreements on the Promotion and Protection of Investment and the establishment of Joint Business Council between Oman and Tanzania. Surely, these will go a long way towards reducing further the risk of investing in Tanzania and promoting business relations. I hope our two governments will conclude at the earliest possible time, ongoing the negotiations on the avoidance of double taxation.

Market-based Economy with Stable Macroeconomic and Fiscal Policy Regime

Ladies and Gentlemen;

Tanzania espouses market based economic policies. This is very much a function of economic reforms we have been undertaken since the mid-1980s. As you may know, prior to that Tanzania espoused socialist policies. All commanding heights of the economy were in the hands of the state. The state was involved in the production and distribution of goods and services from village to national level. The state also continued to perform the traditional functions of maintaining law and order and, governing with the advent of economic reforms a fundamental policy decision was made. This was about the government doing the primary functions of the state of governing and maintaining law and order, leaving the private sector to do business.

Briefly, the new policy could be summarized as follows, let “Government Govern and Private Sector do Business”. In pursuit of this new policy the government began to withdraw from direct involvement in production and distribution activities and left them in the hands of the private sector. A comprehensive programme of divestiture of state enterprises followed. Todate, most state enterprises have been privatized except for a few public utilities in the sector of water, electricity, railways, roads, health and education. Even with these sectors, the private sector is allowed direct involvements. The government still owns the state enterprises although in some aspects there is private sector participation.

The economic reforms have worked well for the Tanzanian economy despite some challenges. The economy has turned around from the stresses and downward trends before the reform. The macro-economic frame back on track and benefits are being enjoyed. Tanzania today enjoys macro-economic stability. All macro-economic indicators are good and at the seven percent average economic growth rate over the past decade, Tanzania is among the 20 fastest growing economies in the world. Currently, due to high food and oil prices, inflation has been a challenge. However, there are positive signs of decline, from 19.5 percent three months ago to 14.9 percent last month. We hope to get back to single digit by June, 2013.

Geographical Location

Ladies and Gentlemen;

Tanzania is strategically located in the eastern coast of Africa so, come and invest to take advantage of it. Tanzania borders eight countries of Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Democratic Republic of Congo, Zambia, Malawi and Mozambique. It is a gateway for six landlocked countries Zambia, Malawi, Rwanda, Democratic Republic of Congo, Burundi and Uganda which use Tanzanian ports, roads, railways for their import and export trade. Tanzania is also the gateway for goods to and from Eastern DRC. In this regard, therefore, investments or businesses to cater for the facilitation of imports and exports of these countries present lucrative opportunities.

One can invest in lucrative freight related businesses like clearing and forwarding, warehousing, logistic centres, trucking business etc. But there are also opportunities in port development and management, building toll roads, railways, air transportation etc.

This location also presents ample opportunities for situating manufacturing and trading businesses in Tanzania. There is almost a captive market to take advantage off. Fortunately, also Tanzania shares regional economic grouping with all these countries. As such, locating your businesses in Tanzania enables you to access the East African Community market of 120 million people which are in Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi. You can also access close to 200 million people market of the Southern African Development Community, with the DRC, Zambia, Malawi, Mozambique, Angola, Namibia, South Africa, Zimbabwe, Lesotho, Swaziland, Mauritius, Seychelles and Madagascar. In these two economic groupings there is free movement of goods and services. There is discussion going on between East African Community, SADC and COMESA of creating free Trade Area. This boasts population of close to 540 million and USD 1trillion GDP.

Ladies and Gentlemen;

Besides its geography Tanzania itself presents abundant investment opportunities in agriculture, mining, tourism, manufacturing, fishing, ICT, and infrastructure development. In agriculture there is plenty of arable land yet to be utilized, the climate is permissive and there are adequate water resources for irrigation. In mining nearly all minerals known to exist in the earth crust also do exist in Tanzania and some in large qualities. Of recent, with the new discoveries of sizeable natural gas deposits, it makes Tanzania to be a prospective an emerging market for gas production in the world.

In the hospitality industry with the beautiful and historic spice Islands of Zanzibar and exotic world renown game parks, on the mainland. Tanzania is a tourist destination worthy investing now and in future. With the huge lakes and 1000 km of sea coastline and the 200 km EEZ, fishing is a highly prospective investment opportunity. Right now there is no serious fishing in our sea.

There are limitless opportunities in infrastructure development, telecommunications, power generation, railways, ports development, airports, airlines etc. With a huge raw material base from agriculture, mining, fishing and forestry investments in manufacturing present huge potential. There is, as mentioned earlier, a sizeable own market of close to 45 million people, 120 million people East African Community and 200 million people of SADC market. But we also have market access arrangements with the USA under AGOA, European Union (Everything but arms), China and Japan which makes investing in Tanzania even more attractive.

Skilled Labour Force

Ladies and Gentlemen;

Tanzania, also boasts of having sizeable population of skilled labour force. Over the years, we have invested substantially in education at all levels, from primary to secondary school and higher learning. We have also expanded vocational education and established training centres in every region of the country. These have been useful in training highly qualified experts in many fields as well as technicians and artisans in various trades. While we have invested heavily in education to develop the local talent, we are keen on working with businesses on innovative ways to develop the local talent that is relevant to the specialized areas of interest. It is important to note also that labour in Tanzania is relatively less expensive compared to many other parts of the world.

Ladies and Gentlemen;

The business climate that I have just described has already attracted growing number of foreign and local investors from different countries to Tanzania. Oman is also included in that list as between 2000 to 2011, Omani investors have registered 36 projects worth more than USD 200 million in different sectors. This is not much compared to what can be availed by Omani business community. We look forward to increased investments because as I mentioned, opportunities are many. The returns are good, protection is guaranteed and incentives are really competitive. We also look forward to increasing trade between Tanzania and Oman, which is currently very low.

So I warmly welcome you to come to Tanzania and explore the unlimited, trade, investment and business opportunities which our country has to offer.

Ladies and Gentlemen;

Those interested in investing in the manufacturing business can take advantage of the opportunities which exist in the various Export Processing Zones (EPZ) and the Special Economic Zones (SEZ) which we have set up to promote and facilitate industrial development and export of manufactured goods to the worlds. We cannot continue to be exporter of raw materials. We want to add value to our primary products. We will support all those of you who will opt to operate in these designated zones.

Ladies and Gentlemen;

Let me conclude by saying the following. First, Tanzania meaning both Zanzibar and Tanzania Mainland is ready to do business with you. Our doors are wide open. Secondly, Tanzania have everything that you need to look for in taking a decision about where to invest: conducive business environment, political sound economic policies, macro-economic stability, abundant natural resources, relative educated labour-force, a sizeable and captive market because of Tanzania’s unique geographical location. Above all, the government is facilitative. The list is long, I can hardly exhaust it. As mentioned earlier these will be elaborated further in the course of your discussions by the representatives of the Tanzania Investment Centre (TIC) and the Zanzibar Investment Promotion Authority (ZIPA) who are here with us.

Several ministers are also here to clarify on some of these issues and concerns. Above all, business men and women from Tanzania are also here to share their experiences and expectations.

After those many words, I declare the Tanzania – Oman Business Forum is officially open. I thank you for listening and wishing you very successful deliberations.

Thank you very much and God bless you.

Rais Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika Taifa la Kifalme la Oman, Sultani Qaboos wa Oman amtunuku nishani ya Heshima

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi mwenyeji wake Sultani wa Oman Qaboos bin Said Al Said katika kasri ya AL Alam jijini Muscat Oman jana jioni muda mfupi kabla ya dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa kwa heshima yake.

 Sultani wa Oman,Qaboos bin Said Al Said akimtunuku Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete nishani ya juu ya heshima, Taifa la Oman wakati wa dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima ya Rais Kikwete na ujumbe wake jana jioni katika kasri ya  AL Alam jijini Muscat Oman.

Sultan Qaboos bin Said Al Said akimpongeza Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumtunuku nishani ya juu ya heshima ya Taifa la Oman jana jioni katika kasri ya AL Alam. Jijini Muscat Oman jana jioni .Rais Kikwete aliwasili nchini Oman jana jioni kwa ziara rasmi ya siku nne. Picha na Freddy Maro

Juu: Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mwenyeji wake Sultani wa Oman Qaboos bin Said Al Said katika kasri ya Sultani jijini Muscat. Chini  Watoto  wakitanzania ambao wazazi wao wanaishi na kufanya kazi katika ubalozi wa Tanzania nchini Oman wakimkaribisha kwa maua Rais Dkt.Jakaya Kikwete muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa  Muscat jana jioni.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Sultani wa Oman Qaboos bin Said Al Said wakipokea heshima za viongozi muda muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili jijini Muscat Oman leo mchana kwa ziara rasmi (State Visit) ya siku tatu nchini Oman.

 


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mwenyeji wake Sultani wa Oman Qaboos bin Said Al Said katika kasri la Sultani jijini Muscat leo. Picha na Freddy Maro

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika Taifa la Kifalme la Oman, ikiwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.
Rais Kikwete na ujumbe wake ameondoka mjini Dar es Salaam asubuhi ya leo, Jumatatu, Oktoba 15, 2012, kwenda Oman kuanza ziara hiyo inayofanyika kwa mwaliko wa Kiongozi wa Ufalme wa Oman, Mfalme Qaboos bin Said, ambaye atakuwa mwenyeji wake kwa siku zote nne.
Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Muscat, Rais Kikwete anatarajiwa kulakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Mheshimiwa Yousef bin Abdullah bin Alawi ambaye ataandamana naye hadi Jumba la Muscat Gate ambako Rais atapokelewa na Mfalme Qaboos. Kutoka hapo wataandamana hadi Kasri ya Kifalme ya Al Alam ambako atapokelewa rasmi kwa heshima zote za Kiserikali.
Shughuli kubwa ya jioni ya leo ya Mheshimiwa Rais itakuwa ni kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Serikali za Tanzania na Ufalme wa Oman na pia kuhudhuria dhifa rasmi ambayo Mfalme Qaboos atamwandalia mgeni wake kwenye Kasri ya Al Alam.
Kesho, Jumanne, Oktoba 16, 2012, Rais Kikwete atatembelea Jumba la Makumbusho la Majeshi ya Ulinzi ya Oman, atafungua Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Oman, atashuhudia utiaji saini makubaliano ya mikataba miwili kati ya nchi hizo mbili, ukiwamo ule wa kuundwa kwa Baraza la Biashara la Tanzania na Oman na ule wa Kuendeleza na Kulinda Uwekezaji katika nchi hizo mbili.
Jioni, Rais Kikwete atatunukiwa nishani ya juu kabisa ambayo Ufalme wa Oman hutoa kwa viongozi wa nchi za nje ya First Order Medal kwenye Chakula Maalum cha Usiku kitakachoandaliwa na Mfalme Qaboos kwa heshima ya Rais Kikwete.
Rais Kikwete na ujumbe wake pia utakutana na kuzungumza na Watanzania wanaoishi Oman katika mkutano utakaofanyika kwenye Hoteli ya Kifalme ya Al Bustan.
Hii itakuwa mara ya pili kwa Mheshimiwa Kikwete kutembelea Oman. Aliitembelea nchi hiyo mara ya kwanza mwaka 1998, wakati huo akiwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Rais Kikwete katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu, Kampala, Uganda

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika Mkutano wa Viongozi wa nchi za Maziwa Makuu
 katika ukumbi wa mikutano wa Munyonyo Commonwealth Resort jijini Kampala leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taif Mhe. Shamsi Vuai Nahodha (kulia kwake) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamaha wakielekea kwenye mkutano wa viongozi wa nchi za Maziwa Makuu wanaokutana katika ukumbi wa mikutano wa  Hoteli ya Speke Resort Munyonyo jijini Kampala Septemba 8, 2012.

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi makubaliano yaliyofikiwa na Wakuu wenzake wa Nchi na Serikali za Ukanda wa Maziwa Makuu baada ya mkutano wao uliofanyika Septemba 8, 2012 katika Hoteli ya Speke Resort Munyonyo mjini Kampala, Uganda.

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipitia waraka wenye makubaliano kabla ya yeye na Wakuu wenzake wa Nchi na Serikali za Ukanda wa Maziwa Makuu kuuweka sahihi baada ya mkutano wao uliofanyika Septemba 8, 2012 katika Hoteli ya Speke Resort Munyonyo mjini Kampala, Uganda.  
Rais Jakaya Mrisho Kikwete azungumzia juhudi za kupatikana kwa amani ya kudumu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) baada ya mkutano wa viongozi wa nchi za maziwa makuu kilichofanyika Kampala, Uganda, Septemba 8, 2012

Rais Jakaya Kikwete atoa heshima za Mwisho kwa Meles Zenawi, asaini kitabu cha maombolezo, aweka shada la maua

 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo leo  ikulu ya Addis Ababa
kufuatia kifo cha Waziri Mkuu wa Ethiopia Marehemu Meles Zenawi anayetarajiwa kuzikwa kesho.
Wengine katika picha ni baadhi ya wajumbe waliofuatana na Rais Kikwete watakoshiriki mazishi ya kiongozi huyo.
Kutoka kushoto ni Mbunge wa Mtera Mhe.Livingstone Lusinde, Aliyewahi kuwa balozi wa Tanzania nchini
Ethiopia Jenerali Mirisho Sarakikya, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe.Joram Boswaro,
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe.Zitto Kabwe na Waziri wa Kazi wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman.

Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiweka shada la maua na kutoa heshima zake mwisho kwa aliyekuwa
Waziri mkuu wa Ethiopia Marehemu Meles Zenawi katika Ikulu  ya Addis Ababa jioni hii
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akito heshima zake mwisho kwa aliyekuwa Waziri mkuu wa
Ethiopia Marehemu Meles Zenawi katika ikulu  ya Addis Ababa jioni hii
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akikutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Waziri MKuu wa
Ethiopia Mhe. Hailemariam Dessalegn jijini Addis Ababa jioni hii. Picha na Freddy Maro

RAIS KIKWETE AOMBOLEZA KIFO CHA WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA HAYATI MELES ZENAWI

MAREHEMU MELES ZENAWI

          Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya leo, Jumanne, Agosti 21, 2012, amepokea kwa mshtuko mkubwa, masikitiko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mheshimiwa Meles Zenawi, kilichotokea jana usiku nje ya nchi ambako alikuwa anatibiwa.

Kufuatia taarifa hizo, Mheshimiwa Rais Kikwete, kwa niaba ya wananchi wa Tanzania, Serikali yake na kwa niaba yake mwenyewe amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Ethiopia, Mheshimiwa Girma Wolde-Giorgis. 
Katika rambirambi zake kwa Mheshimiwa Wolde-Georgis, Rais Kikwete amesema: “Tanzania imepokea kwa mshtuko mkubwa, masikitiko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Mheshimiwa Meles Zenawi  kilichotokea jana usiku.”
Amesema Rais Kikwete: “Kwa niaba ya wananchi wa Tanzania, Serikali yangu na mimi mwenyewe, natuma salamu zangu za dhati za rambirambi kwako, kwa wananchi wa Ethiopia na kupitia kwako kwa Mheshimiwa Azeb Mesfin, mjane wa marehemu na familia nzima ya Mheshimiwa Meles Zenawi. Tupo nanyi katika msiba huu mkubwa.”
“Kwa hakika, Ethiopia imempoteza kiongozi hodari, mwana mapinduzi na mpenda maendeleo. Kwa hakika,  Afrika imempoteza kiongozi wa kutumainiwa na msemaji hodari sana wa Bara letu. Daima tutamkumbuka Waziri Mkuu Zenawi kwa msimamo wake thabiti wa kutetea maslahi ya Afrika na ustawi wa watu wake. Mimi na Tanzania tumempoteza rafiki wa kweli” amesema Rais Kikwete na kusisitiza, “hakika tutaukosa mchango wake uliojaa busara, hoja zake za kusisimua na zenye mantiki sana.”
Rais Kikwete amemaliza kwa kuwaeleza wananchi wa Ethiopia: “Tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu wa majonzi na tunamwomba Mwenyeji Mungu awape nguvu, moyo, subira na baraka zake ili muweze kuvuka kipindi hiki. Aidha, tunaungana nanyi na familia ya Marehemu Zenawi kumwomba Mola ampe mapumziko mema Marehemu Meles Zenawi.”
Waziri Mkuu Zenawi ambaye ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 57 amekuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia tokea 1995 na kabla ya hapo alikuwa Rais wa nchi hiyo kati ya 1991 na 1995.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
21 Agosti, 2012

Rais Jakaya Mrisho Kikwete arejea kutoka Msumbiji

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe raymond Mushi baada ya kureje usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikohudhuria kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja Kwa zamu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikohudhuria kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja  

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe Sophia Mjema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikoambatana na Rais Kikwete katika  kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja. PICHA NA IKULU

Rais Dkt.Jakaya Kikwete na Rais Joyce Banda wa Malawi wakutana Msumbiji na kuzungumzia Mgogoro wa mpaka

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na Rais wa Malawi Mhe. Joyce Banda mjini Maputo Msumbiji leo asubuhi kuzungumzia kutafuta suluhu katika mgogoro wa mpaka kati nchi hizo uliopo kwenye ziwa Nyasa.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais wa Malawi Mhe. Joyce Banda na wameelezea nia ya nchi zao kufikia suluhu kwa njia za kidiplomasia kupititia kamati maalumu iliyoundwa kushughulikia mgogoro huo (picha na Freddy Maro).

ACCEPTANCE SPEECH BY H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, ON ASSUMING THE CHAIRMANSHIP OF THE SADC ORGAN ON POLITICS, DEFENCE AND SECURITY COOPERATION

17TH AUGUST, 2012, MAPUTO, MOZAMBIQUE

 Your Majesty, King Mswati III of the Kingdom of Swaziland;

Your Excellency Armando Guebuza, SADC Chairperson and President of the Republic of Mozambique;

Your Excellency Madam Joyce Banda, Deputy Chairperson of SADC and President of the Republic of Malawi;

Your Excellency Hifikepunye Pohamba Deputy Chairperson of the SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation and President of the Republic of Namibia;

Fellow Heads of State and Government; Heads of Delegations;

Your Excellency Dr. Tomaz Augusto Salomao, SADC Executive Secretary;

Honourable Ministers; Permanent Secretaries;

Ambassadors and High Commissioners;

Distinguished Delegates;

Ladies and Gentlemen;

It is with a great sense of humility and gratitude that I stand before this august assembly to do two things.  To move a vote of thanks on behalf of all of  us and to thank you for the honour you have reposed on me and my country. On behalf of the government and the people of the United Republic of Tanzania, I sincerely thank my fellow Heads of State and Government and the entire SADC family for choosing Tanzania to Chair the SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation for the coming one year.

We are very much aware that this is not an easy task in view of the political, peace and security challenges facing our region at the moment and the ones we cannot predict that could happen in future.  However, I am comforted by the fact that the work of this Organ is a shared responsibility.  You have entrusted me and my country with the unenviable role of a coordinating our collective efforts in the search for solutions to the political, diplomatic and security issues of concern to individual member states and our region as a whole.

Your Majesty;

Excellencies, Distinguished Participants;

          My promise to you all today is that we will do our utmost to live up to your expectations.  With the sterling work done by my predecessor and continued collective efforts and support from all of us, we will overcome the challenges we face and advance to greater heights. 

Allow me to pay glowing tribute to the outgoing Chair, my dear brother and good friend, His Excellency Jacob Zuma, President of the Republic of South Africa, for steering so well the affairs of the Organ in the past one year. We are grateful for his outstanding leadership, dedication and commitment to the work of the Organ during his tour of duty.   Surely, we will benefit and build on the good work he and other members of the Troika Organ have done.  I also thank, the President of the Republic of Zambia, His Excellency Michael Sata, the outgoing member of the Troika, for being a highly dependable partner. He and his government have made an enviable contribution to the work of the SADC Organ and its achievements.  We will surely miss his charm and candidness.

Excellencies;

Tanzania is picking the baton of leadership of the SADC Organ on Politics, Defence and Security at a time when a lot of ground has been covered with regard to the crisis in Madagascar.  Perhaps what remains of us now, is to run the last mile. Unfortunately, it appears to be on too steep a climb, making it complicated to negotiate and almost elusive to resolve.  We will not and should not tire nor give up until a lasting solution is found.

Likewise, remarkable progress has been made in Zimbabwe, with regard to advancing reconciliation, the process of constitution making and preparing the ground for the next elections. I want to assure this august assembly of Heads of State and Government that the Troika of the SADC Organ will work hand in glove with the Troika of SADC and the rest of us to consolidate the gains made and advance from where President Jacob Zuma left off.   We will also work with all stakeholders in Zimbabwe to ensure successful conclusion of the process of drawing up the new Constitution and ensure that the coming elections are democratic, free and fair.

In the same vein, we will work closely with other members of the troika of SADC Organ on Politics, Defence and Security to oversee SADC’s active involvement in finding peaceful resolution of the crisis in the Eastern Democratic Republic of Congo. The ongoing security and humanitarian crises in this member state of our Organization is very disturbing and unacceptable. The Congolese people have suffered for far too long.  They deserve to get a break and live better.  It is high time that the crises ended forever and they are left to concentrate on more positive and productive activities of improving their living standards. SADC has a unique role to play and Tanzania feels privileged to be afforded the opportunity to coordinate these noble efforts.

Mr. Chairman;

Ladies and Gentlemen;

As we continue to get involved in the affairs of the DRC, we are cognisant of the work being done under the framework of the International Conference on Great Lakes Region (ICGLR). Four SADC member states namely Angola, DRC, Zambia and Tanzania are members of the ICGLR as well.  This is very opportune indeed, for our Organisation because these countries will be SADC’s bridge to advance our cause, ideas and positions.  It is in our mutual interest for SADC to work closely with the ICGLR in this regard.

Mr. Chairman;

Ladies and Gentlemen;

I would like to take this opportunity to congratulate Her Excellency Dr. Nkosazana Dlamini Zuma, for being elected the Chairperson of the African Union Commission (AUC).  Emerging victorious in a highly contested election like the one held in July 2012 in Addis Ababa, is a matter she and our region deserve a lot of praise. We have every reason to congratulate her and ourselves.

Indeed, Madam Nkosazana Zuma has re-written AU’s history in two ways.  First, she is the first woman ever to hold that prestigious high office of our continental organization for the past 49 years.  And, second, it is the first time for Southern Africa to get the opportunity to hold this office.  It is, indeed, a great pride for the SADC region because our concerted efforts and perseverance have paid off handsomely. I take this opportunity to acknowledge and thank our Ministers for Foreign Affairs for a job very well done. Madam Nkosazana Zuma has made us proud.  We wish her every success and assure her of our unwavering support and cooperation.

Excellencies;

On behalf of all Heads of State and Government and all delegates to this 32nd SADC Summit, I would like to take this opportunity to thank most sincerely President Armando Emilio Guebuza and the great people of this country for the warmth of reception and gracious hospitality. We have been enjoying every minute of our stay.  You have made us feel very much at home.  You have provided excellent facilities for our meeting at this magnificent Joaquim Chissano International Conference Centre.

We thank you so much for your very able stewardship of our meeting yesterday and today.  We are confident that under your excellent leadership, SADC is in very safe hands and bound to make great strides.  With you in the chair we look to the future with great hopes and optimism.  On behalf of all colleagues, we promise you unqualified support and cooperation.

It would be remise of me if I did not acknowledge and commend the SADC Secretariat under the able leadership of Dr. Tomas Salomao, the Executive Secretary, for a job very well done.  You have made excellent preparations for this meeting which made the work of the Summit smooth and easy.  Please keep up the good work.

Let me conclude by saying that SADC is an organisation with great prospects now and in future.  I am confident that together we shall deliver on our promise and the expectations of the people this Organisations is supposed to serve.

Last but not least, I would like to use this opportunity to remind you of my invitation to all SADC Heads of State and Government to attend the Smart Partnership Dialogue to be held in Dar es Salaam between 24th – 28th May, 2013.  The theme is very pertinent and relevant to the challenges of development we are grappling with every day: “Leveraging Modern Technology for Africa’s Development”  I expect all of you to attend.

`

Thank you for your attention. Muito obrigado!

 

 

RAIS KIKWETE AONANA NA RAIS MPYA WA GHANA, ATEMBELEA MASHAMBA YA MANANASI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Rais John Dramani Mahama wa Ghana nyumbani kwake jijini Accra leo Agosti 11, 2012 baada ya kumtembelea na kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Marehemu John Evans Atta Mills aliyezikwa jana.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais John Dramani Mahama wa Ghana nyumbani kwake jijini Accra leo Agosti 11, 2012 wakati alipomtembelea kiongozi huyo mpya wa Ghana na kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Marehemu John Evans Atta Mills.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitazama manasi yakitayarishwa kwa ajili ya kusafirishwa na kuuzwa nje ya nchi katika kiwanda cha Bomarts Farms Ltd. katika kitongoji cha Dobro nje kidogo ya jiji la Accra leo Agosti 11, 2012.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitazama ukulima wa kisasa wa manasi yanayolimwa kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi katika shmaba la Bomarts Farms Ltd. katika kijiji cha Dobrokatika eneo la Nsawam nje kidogo ya jiji la Accra leo Agosti 11, 2012. Kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa shamba hilo Bw. Anthony Botchway na mwenye suti ya buluu ni Waziri wa Chakula na Kilimo Mhe Kwesi Ahwol.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia upandaji wa miche ya mananasi katika shamba la Koranco kijiji cha Obotweri nje kidogo ya jiji la Accra. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Koranco Farms Ltd. Bw Emmanuel B. Koranteng ambaye amekuwa akilima shamba la matunda kwa miaka 27. Mwalimu Nyerere aliwahi kumtembelea shambani hapo katikati ya miaka ya 1980 kujionea ukulima huo wa matunda.PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE KATIKA MAZISHI YA RAIS JOHN ATTA MILLS WA GHANA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo wakati shughuli ya mazishi ya Rais John Evans Atta Mills wa Ghana katika ukumbi wa Mikutano wa Ghana jijini Accra leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Rais wa Ghana Marehemu Profesa John Evans Atta Mills katika ukumbi wa Mikutano wa Ghana jijini Accra leo.
Shughuli mbalimbali za mazishi za aliyekuwa Rais wa Ghana Profesa John Evans Atta Mills katika uwanja wa Independence Square jijini Accra leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na viongozi wenzie baada ya shughuli ya mazishi ya Rais John Evans Atta Mills wa Ghana jijini Accra leo.
Jukwaa kuu katika uwanja wa Independende Square wakati wa Shughuli mbalimbali za mazishi za aliyekuwa Rais wa Ghana Profesa John Evans Atta Mills katika uwanja wa Independence Square jijini Accra leo.PICHA NA IKULU.

Rais Kikwete arejea Nyumbani baada ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za maziwa Makuu

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Mwenyekiti wa Mkutano wa wakuu wa nchi za Maziwa Makuu,Rais Yower Kaguta Museveni wa Uganda mwishoni mwa mkutano huo uliomalizika leo jijini Kampala Uganda.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini maazimio ya wakuu wa nchi za Maziwa Makuu mwishoni mwa mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Speke’s Bay Resort,Munyonyo, KaMPALA, Uganda.
Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe na Meya wa Jiji la Dar es Salaam Dkt.Didas Masaburi wakimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea jijini Kampala Uganda ambapo alihudhuria mkutano wa wakuu wan chi za Maziwa Makuu(picha na Freddy Maro).

Rais Kikwete, Museveni,Kagame,na Rais Kabila wakutana jijini Kampala katika mkutano wa Maziwa Makuu

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Paul Kagame wa Rwanda(kushoto),Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda(Watatu kulia) na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo wakiwa katika mkutano wa viongozi wan chi za Maziwa Makuu unaofanyika jijini Kampala Uganda leo jioni.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wakifurahia  jambo wakati wa mkutano wa Viongozi wa nchi za Maziwa Makuu unaofanyika jijini Kampala Uganda. Picha na Freddy Maro

RAIS KIKWETE AELEKEA NCHINI UGANDA LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rubani Bomani na wanaanga wenzie wa Ndege za Serikali kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuuasubuhi leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Mecky Sadik kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda,kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuu asubuhi leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi la Tanzania Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo kabla ya kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuuasubuhi leo. Katikati yao ni Inspoekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema.PICHA NA IKULU

Rais Kikwete ahudhuria mazishi ya shemeji yake mjini Lindi leo

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo amehudhuria mazishi ya shemeji yake, Marehemu Amani Kinyozi (45), aliyefariki Jumamosi iliyopita jijini Dar es salaam, na kuzikwa katika makaburi ya Mitandi mjini Lindi.Pichani ni Rais Kikwete akishiriki katika swala ya kumuombea marehemu mjini Lindi leo.

Rais Kikwete akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya shemeji yake, Marehemu Amani Kinyozi, katika makaburi ya Mitandi mjini Lindi leo Julai 30, 2012.PICHA NA IKULU.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Jakaya Mrisho Kikwete, amewasili mjini Lindi leo, Jumatatu, Julai 30, 2012 kwa ziara ya siku mbili ambako miongoni mwa mambo mengine atafuturisha wananchi na viongozi wa mkoa wa Lindi.

Aidha, rais Kikwete amehudhuria mazishi ya shemeji yake , Marehemu Amani Kinyozi, aliyefariki siku ya Jumamosi jijini Dar es salaam.

Rais Kikwete, ambaye ameongozana na mke wake Mama Salma Kikwete, alijumuika na mamia ya wakazi wa mji wa Lindi kwenye mazishi hayo, yaliyofanyika katika makaburi ya Mitandi, mjini humo.

Marehemu Amani Kinyozi, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 45, ameacha mke na watoto wawili.

Enzi za uhai wake marehemu alikuwa mtaalamu wa kutengeneza mifuko ya karatasi, na pia alikuwa akifundisha kinamama wajasiriamali ufundi huo katika juhudi za kuepukana na matumizi ya mifuko ya plastiki, maarufu kama mifuko ya rambo ya kufungia bidhaa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
30 Julai, 2012

Rais Kikwete ahudhuria Mkutano wa Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihudhuria kikao cha Ulinzi na Usalama cha Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa Ethiopia. Kulia ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabbwe
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na kiongozi wa ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini China Bwana Quan Zhezhu wakati walipokutana jijini Addis Ababa Ethiopia.
Rais Dkr.Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na ujumbe wa wafanyabiashara wakubwa kutoka China.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akijadiliana jambo na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe(kulia) pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe. Joram Biswaro(Katikati) wakati wa kikao maalimu cha nchi za Maziwa Makuu kilichofanyika sambamba na Mkutano wa 19 wa Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika AU jijini Addis Ababa Ethiopia

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Rais wa Sudan Omar Hassan el  Bashir wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika unaoendelea jijini Addis Ababa Ethiopia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine wanchi  za Afrika wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 19 wa wakuu wan chi za umoja wa Afrika(AU) jijini Addis Ababa Ethiopia leo. 

Picha na mdau  Freddy Maro wa Ikulu


Rais Kikwete awasili jijini ddis Ababa Ethiopia kuhudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Umoja wa Afrika AU

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea maua muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa Ethiopia kuhudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Umoja wa Afrika AU leo jioni.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili jijini Addis Ababa Ethiopia kuhudhuria mkutano wa 19 wa  wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika leo jioni.Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe na kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe.Joram Biswaro Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu.

President Kikwete arrives in London for a ground breaking International Family Planning Summit

President Jakaya Mrisho Kikwete is received at the Regency Hyatt Churchhill hotel in London today July 10, 2012 ready to attend a two-day a ground breaking International Family Planning Summit. The Summit is scheduled to launch a Global Movement to give an additional 120 million women in the World’s poorest countries, access to lifesaving family planning information, services and supplies by 2020.

The United Kingdom’s Government and the Bill & Melinda Gates Foundation, with the support of UNFPA and other partners, are hosting the summit, whose envisaged increased access will enable these women and girls to choose whether, when and how many children to have.

This Summit is a collective opportunity to generate global commitments to increase access to family planning and, in doing so, accelerate the achievement of MDGs 4 (reducing child mortality) and 5 (improving maternal health) – including MDG target 5b (reproductive health) – as well as MDG target 6a (HIV prevention).

It will build on the momentum created by the UN Secretary General’s Global Strategy for Women’s and Children’s Health, “Every Woman, Every Child”, and the innovative public-private and civil society partnerships that are developing through the Reproductive Health Supplies Coalition (RHSC) and their Hand to Hand Campaign.

Leaders from developing and developed countries, donors, civil society groups and the private sector will come together behind a simple vision: to give women in the developing world the same access to lifesaving family planning as women in the developed world.

PHOTO BY STATE HOUSE

President Kikwete to submit Tanzania governance report to AU

By Special Correspondent

President Jakaya Kikwete of Tanzania is set to present Tanzanian governance report to the meeting of the African leaders participating in the African Union governance assessment body-the African Peer Review Mechanism (APRM) next January.

The information was revealed yesterday by the APRM Tanzania chapter Head of Communications and Media Relations, Hassan Abbasi when briefing reporters at the on-going Dar es Salaam International Trade Fair.

“As our focal point Minister of Foreign Affairs, Hon Bernard Membe said recently, the report which was supposed to be presented by the President this July had to be postponed to January,2013 following the APRM Continental Secretariat’s failure to finish the report in time,” said Mr. Abbasi.

He added that the Tanzanian APRM chapter received new communication from the Continental Secretariat which is based in Midrand in South Africa informing that the report was ready but willl be first discussed internally by a group of African eminent persons for quality assurances.

“Our fellows have confirmed to us that now the report on state of governance in Tanzanians and the expert recommendations thereof is ready and awaits quality review from top African eminent persons who will meet on 11-12 July in Addis Ababa,” added Mr. Abbasi.

He revealed that the report will hint on the country’s governance in four thematic areas of democracy and political governance, economic management, corporate governance and socio-economic development as per Tanzanians views collected from various stakeholders.

March this year when launching the Country Review Team in Dar es Salaam, President Kikwete promised to implement recommendations under the APRM process.

“APRM is like a mirror that helps us to see ourselves where we are and what we have achieved in terms of ensuring democratic leadership and good governance and economic development in our countries.

“It is against this truth that we are more than ready to implement your recommendations when the right time comes,” said the President in March. The Review team left Dar es Salaam on 23 March after three weeks of consultations with both state and non-state actors in Tanzania and promised to present their review report by May, 2012 however the process took much longer.

Tanzania is currently among 32 out of 54 African countries participating in the APRM process which is repeated every after four years to assess governance among member states. APRM was initiated in 2003 by African Heads of State and Government. Tanzania joined in 2004 and kick started the process in 2007.

Rais Kikwete akutana na Rais Kabila pamoja na Naibu Waziri Mkuu wa Ubelgiji

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo(DRC) mjni Bujumbura Burundi ambapo walifanya mazungumzo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Naibu Waziri mkuu wa Ubelgiji Bwana Didier Reynders mjini Bujumbura Burundi leo baada kufanya mazungumzo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Katibu mkuu wa Maziwa Makuu Professa Ntumba Luaba Alphonse mjini Bujumbura Burundi leo(picha na Freddy Maro).

Rais kikwete ahudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Burundi mjini Bujumbura leo

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakiwa pamoja na viongozi wengi ne waliohudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Burundi mjini Bujumbura leo. Kutoka kushoto ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rais Teodoro Nguema wa Equatorial Guinea,Mwenyeji Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi na mkewe na Rais Mwai  Kibaki wa Kenya

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakifurahia jambo wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Burundi yaliyofanyika mjini  Bujumbura leo.Kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.Picha na Mdau Freddy Maro wa Ikulu

Rais Kikwete na mama Salma wahudhuria sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Rwanda

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mwenyeji wake Rais Paul Kagame wa Rwanda wakipokea haeshima za marais muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kigali kuhudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Rwanda leo asubuhi.

 Rais dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Paul Kagame wa Rwanda wakikagua gwaride la  heshima katika uwanja wa ndege wa Kigali.

 Rais Paul Kagame wa Rwanda akimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete katika uwanja wa michezo wa Amahoro mjini Kigali Rwanda kwaajili ya sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Rwanda.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Paul Kagame wa Rwanda wakiteta jambo wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Rwanda zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa Amahoro jijini Kigali leo asubuhi. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu

STATEMENT BY H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE OFFICIAL LUNCHEON IN HONOUR OF H.E. MOHAMED ABDELAZIZ, PRESIDENT OF THE ARAB DEMOCRATIC REPUBLIC OF SAHARAWI, AT THE STATE HOUSE DAR ES SALAAM, 25TH JUNE, 2012

Your Excellency Mohamed Abdelaziz, President of the

      Saharawi Arab Democratic Republic;

Honourable Bernard Kamillius Membe MP, Minister for

       Foreign Affairs and

International Co-operation;

Excellencies Ambassadors and High Commissioners;

Invited Guests;

Ladies and Gentlemen:

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, it is my pleasure to welcome Your Excellency and the esteemed members of your delegation toTanzania, and in particular toDar es Salaam, the Haven of Peace.   I sincerely thank you Mr. President for accepting the invitation to pay us a visit. Indeed, we feel greatly honored and privileged to welcome you in our country. Please feel at home and enjoy your short stay inTanzania.

Excellencies;

Ladies and Gentlemen;

The relationship between the Arab Democratic Republic of Saharawi andTanzaniais historical and has been consolidated by our firm

support to the cause of the liberation of Africa and the right of the people of Western Sahara’s to self-determination.  To our founding fathers of our nation the right to self-determination is a just cause and a principle that we have always cherished.   It is the same principle that guided our country’s position during the liberation struggle of the Southern Africa and other African countries that were under oppression, colonial rule and all the forms of oppression.

        It is this principle that made us host the OAU Liberation Committee and supported the liberation movements morally, materially and diplomatically.  Our support was loud and clear in Africa, the UN, the NAM and other international fora.

Tanzania’s position on the issue of Western Sahara’s independence is a matter of principle. It is based on our conviction on the peoples’ right to self-determination, and on the premise that both the United Nations and African Union have always been unanimous on the need to allow the people of Saharawi to determine their destiny. Several resolutions of the UN and Decisions of the OAU/ AU asserted to that. In December 1965, the UN General Assembly adopted resolution 2072 (XX) which requested Spain to decolonize the territory; thereafter in 1966 the UN requested Spain under resolution number 229 (XX1) to organize, under UN supervision, a referendum on self- determination for Saharawi people. This demand was repeated each year from 1967 to 1973.

Despite all these Resolutions and the International Court of Justice ruling on the legality of self determination, Spain ignored all this and on 14 November 1975, handed the country to Morocco and Mauritania under the Madrid Accord.

Excellencies;

With regards to Western Sahara, Tanzania has been supportive of all UN and OAU efforts and initiatives.  We promise to continue to do so.  We supported the first effort by the Organization African Unity (OAU) to resolve the conflict during the Summit of July 1979 in Monrovia, Liberia, where a mediation initiative for peaceful resolution of Western Sahara conflict was launched. This was followed by the OAU Resolution 103 (XVIII) made in June 1981 in Nairobi, Kenya and Resolution 104 (XIX) reached in Addis Ababa in June 1983. Tanzania was part of the Implementation Committee of the Heads of State on Western Sahara formed to take all measures, with participation of the UN, to guarantee the exercise by the people of Western Sahara of self-determination through a general and free referendum. Since then, the UN and AU have continued to work together to ensure that the referendum is held and that the people of Western Sahara are given the right to decide.

Mr. President;

Tanzaniais following with keen interest the ongoing direct negotiations between the two parties under the mediation of His Excellency Mr. Christopher Ross, the current United Nations Special Envoy.  We believe, it is right thing to do because direct negotiation has a tendency of building an effective partnership and confidence between parties towards a credible political settlement.  It has worked before in many other conflict situations.

I would like to encourage the parties to the conflict to continue with the dialogue until a breakthrough is emerged.  It is only through negotiations that hope of finding an acceptable and lasting solution to both parties is made possible.  On our part, we will support whatever decision you will come up with, as long as it is consistent with international legality, in particular, the principles enshrined in the Charter of the United Nations and African Union. That would ensure a just, legitimate and durable solution.

I implore you to remain positive and open for further negotiation with other party to the conflict. I want to assure you thatTanzaniashall not waiver its support to the cause of the Saharawi people. We will continue to work hard with other peace loving countries in the world to push for a credible political settlement of the conflict within the framework of relevant U.N resolutions and international legality. In this regard, I call upon the international community, particularly the UN and AU to scale up their efforts and resources so that the uncertainty and suffering of Saharawi people comes to an end.

Your Excellency;

It would be remiss of me, if I conclude my remarks without commending you for your commitment and efforts to find a durable settlement to the Saharawi conflict.  I know it is not easy, but I am sure your determination and resolve will continue to lead Saharawi people towards a just solution. I hope your historic visit will open a new page of the relationship that our two countries enjoy.

With these few remarks, ladies and gentlemen, may I now ask all of you present here to rise and join me in a toast: To the continued good health, long life and happiness of President Mohamed Abdelaziz; to the success in the search for peace and prosperity for the people of Sahrawi; to continued friendship, cooperation, and solidarity between the Saharawi people and Tanzanian people.

 I thank you for your kind attention.

President Mohamed Abdelaziz of the Saharawi Democratic Republic concludes his two-day official visit to Tanzania

 President  Jakaya Mrisho Kikwete receives President Mohamed Abdelaziz  of the Saharawi Democratic  Republic HE  Mohamed Abdelaziz at the Dar es salaam State House in Dar es salaam June 25, 2012

 President Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech at a Luncheon he hosted in Honour of  visiting President  Mohamed Abdelaziz at the  Dar es salaam State House

President Kikwete speaks

 A round of applause rings after President Kikwete’s speech

 Nice speech Your Excellency…

President Mohamed Abdelaziz responds 

 President Kikwete and his guest applaud the Tanzania Police Brass band 
 Conductor Inspector Billy Kachale  leads his Brass Band as President Kikwete with his guest look on
 President Kikwete readies to award his guest a special Makonde Chess Board gift
 A special Saharawi gift for President Kikwete
 A symbolic camel  gift for President Kikwete
 Thanks for the  Saharawi robe
A souvenir photo
 President Kikwete escorts his guest 
  
  JKT Cultural troupe
 Guard of Honour
 President Abdelaziz bids farewell to Tanzania’s heads of defence and security
 Fare thee well….
Bon Voyage….

DIFFERENT ACTIVITIES OF PRESIDENT KIKWETE IN WASHINGTON DC

President Jakaya Kikwete talks during a symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. The session outlined key components of the G8 deliverables for food and nutrition security.

President Jakaya Kikwete speaks at the Centre for Strategic and International Studies (CSIS) during a Stateman’s forum on development themed “A country Transformed: A New Agenda for Tanzania”.

President Barak Obama of the United States of America mingles with the crowd after delivering his Keynote Speech at the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete meets UK’s Secretary of State for International Cooperation Hon Andrew Mitchel in the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

US Secretary of State Hillary Clinton for a souvenir wraps up the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete is interviews by radio reporter from the Voice of America’s Horn of Africa services after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Barak Obama of the United States of America introduces President Jakaya Kikwete as he acknowledges the presence of four African leaders present symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. The session outlined key components of the G8 deliverables for food and nutrition security. Others were HE Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia, Prof. John Evans Atta Mills, President of Ghana and African Union Chairman and President of Benin, HE Dr Boni Yayi.

Tanzania’s envoy to the US Ambassador Mwanaidi Sinare Maajar with the Permanent Representative of the African Union to the UN. Ambassador Amina Salum Ali and Senior advisor to the President of Tanzania (Diplomacy) Ambassador Liberata Mulamula take a break after a consultation meeting of leadership on the follow-up of G-8 commitments on the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete and other leaders take part in a consultation meeting of leadership on the follow-up of G-8 commitments on the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete shares a light moment with the USAID Administrator Dr. Rajiv Shah (centre) and the CEO of the Millennium Challenge Corporation Hon Daniel W. Johannes before a heads of state dinner hosted by Chicago Council on Global Affairs after the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Willard InterContinental hotel in Washington DC.

President Jakaya kikwete and the CEO of the Millennium Challenge Corporation Hon Daniel W. Johannes chat with Zanzibar’s Minister for Agriculture and Natural Resources, Mr Suleiman Othman Nyanga before a heads of state dinner hosted by Chicago Council on Global Affairs after the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Willard InterContinental hotel in Washington DC.

President Jakaya Kikwete speaks at the Centre for Strategic and International Studies (CSIS) during a Stateman’s forum on development themed “A country Transformed: A New Agenda for Tanzania”.

Tanzania’s Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives Eng. Christopher Chiza and his Zanzibar counterpart Hon Suleiman Othman Nyanga at the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete meets UK’s Secretary of State for International Cooperation Hon Andrew Mitchel in the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete with Rock Star Bono take part in a live interview with the MSNBC television station after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. Right is NBC’s Andrea Mitchell.

US Secretary of State Hon Hillary Clinton gestures after a group photo with African leaders and the USAID Administrator Dr Rajiv Shah (third right) prior to a reception to celebrate the new partnership to advance food security on the occasion of the G-8 summit at the D. Franklin room at the State Department in Washington DC.

President Jakaya Kikwete with other leaders join US Secretary of State Hillary Clinton for a souvenir photo after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.PHOTOS COURTESY OF THE STATE HOUSE.

RAIS KIKWETE MKUTANONI BRASILIA, BRAZIL,PIA ATEMBELEA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO NA UFUGAJI

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,April 17, 2012 katika mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa meza kuu na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff na wajumbe wengine katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,April 17, 2012 wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership. Kulia ni Waziri wa mambo ya Nje wa Marekani Bi Hilary Clinton.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,  April 17, 2012  kuhudhuria mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Naibu Waziri wa Masuala ya Siasa (AFRIKA) wa Brazil Balozi Paulo Cordeiro de Andrade Pinto jijini Brasilia, Brazil.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu wa Georgie Mh Nika Gilauri katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,baada ya kuhudhuria mkutano wa Open Government Partnership.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Open Government Partnership ukibadilishana mawazo kabla ya ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil. kutoka kushoto ni Waziri katika ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mh Mathias Chikawe, Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Mahadhi J. Maalim na Msahuri wa Rais (Masuala ya Siasa) Dkt Laurian Ndumbaro.

Wajumbe wa Tanzania kutoka taasisi mbalimbali za kiraia na serikali wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na mabalozi wa nchi mbalimbali wakati wa Mchapalo ulioandaliwa na Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mh Francis Malambugi nyumbani kwa Balozi usiku wa April 17, 2012 jijini Brasilia, Brazil.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akijaribu kofia aliyopewa kama zawadi na uongozi wa taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) alipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo kuhusu mashine ya kisasa ya kutambua muda wa kumwagilia maji shambani iliyoundwa na taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu ukulima wa nyanya wa kisasa katika taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA)walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.PICHA NA IKULU.

Rais Kikwete aanza ziara ya kikazi ya siku tano nchini Brazil

q

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Bw Raymond Mbilinyi, baada ya kuwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo
Mke wa Rais Mama Salma kikwete akipokea shada la maua mara baada ya yeye na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo. Kulia kwake ni Rais Kikwete na nyuma kulia ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman na mwenye miwani ni Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Mh Francis Malambugi.
Rais Jakaya Mrisho kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo. Kulia ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.
Rais Jakaya Mrisho kikwete akiongea na Msaidizi Mwandamizi wa Rais (Diplomasia) Balozi Liberata Mulamula baada ya mkutano wa maandalizi ya ziara yake ya siku tano nchini Brazil Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo. katikati ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.

Rais Jakaya Mrisho kikwete amewasili Brazil Jumapili Aprili 15, 2012 kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tano.

Katika ziara hiyo Rais Kikwete anatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Dilma Varna Rousseff wa Brazil na Rais mstasafu wa nchi hiyo Mheshimiwa Inacio da Silva Lula na viongozi waandamizi wa nchi hiyo.

Katika ziara hiyo, Rais Kikwete atahudhuria mkutano wa mwaka wa wakuu wa nchi zinazoshiriki katika Mpango wa Ubia wa Uwazi Serikalini (Open Government Partnership-OGP) utakaofanyika mjini Brasilia chini ya Uenyekiti wa Rais Rousseff na kuhudhuriwa na wajumbe wapatao mia nne (400) kutoka serikalini, Asasi zisizo za kiserikali, Sekta binafsi pamoja na Mashirika ya Kimataifa.

Ubia wa Uwazi Serikalini au kwa kifupi OGP, ni mpango uliozinduliwa Septemba 2011 mjini New York, Marekani kwa lengo la kuwapa wananchi nafasi ya kushiriki katika kuamua mambo yanayowahusu, kupitia vyama visivyo vya Kiserikali na vya Kijamii.

Ubia huu unashirikisha kwa usawa wawakilishi wa serikali kwa upande mmoja na wawakilishi wa Asasi zisizo za Kiserikali za Kijamii kwa upande mwingine. Nchi ya Brazil kwa kushirikiana na Marekani imekuwa mstari wa mbele katika kusukuma ubia huu.

Rais Kikwete anatarajiwa kuhutubia mkutano huo tarehe 17 Aprili, asubuhi mara tu baada ya hotuba ya ufunguzi itakayotolewa na Mwenyekiti wa mkutano huo Rais Dilma Rousseff wa Brazil, ambapo ataelezea maendeleo iliyofikia katika kuandaa mpango kazi wa kutekeleza ahadi ya kuongeza uwazi kama ilivyokubaliwa katika kikao kilichofanyika Disemba 2011.

Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini tarehe 20 Aprili, 2012.