DIFFERENT ACTIVITIES OF PRESIDENT KIKWETE IN WASHINGTON DC

President Jakaya Kikwete talks during a symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. The session outlined key components of the G8 deliverables for food and nutrition security.

President Jakaya Kikwete speaks at the Centre for Strategic and International Studies (CSIS) during a Stateman’s forum on development themed “A country Transformed: A New Agenda for Tanzania”.

President Barak Obama of the United States of America mingles with the crowd after delivering his Keynote Speech at the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete meets UK’s Secretary of State for International Cooperation Hon Andrew Mitchel in the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

US Secretary of State Hillary Clinton for a souvenir wraps up the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete is interviews by radio reporter from the Voice of America’s Horn of Africa services after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Barak Obama of the United States of America introduces President Jakaya Kikwete as he acknowledges the presence of four African leaders present symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. The session outlined key components of the G8 deliverables for food and nutrition security. Others were HE Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia, Prof. John Evans Atta Mills, President of Ghana and African Union Chairman and President of Benin, HE Dr Boni Yayi.

Tanzania’s envoy to the US Ambassador Mwanaidi Sinare Maajar with the Permanent Representative of the African Union to the UN. Ambassador Amina Salum Ali and Senior advisor to the President of Tanzania (Diplomacy) Ambassador Liberata Mulamula take a break after a consultation meeting of leadership on the follow-up of G-8 commitments on the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete and other leaders take part in a consultation meeting of leadership on the follow-up of G-8 commitments on the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete shares a light moment with the USAID Administrator Dr. Rajiv Shah (centre) and the CEO of the Millennium Challenge Corporation Hon Daniel W. Johannes before a heads of state dinner hosted by Chicago Council on Global Affairs after the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Willard InterContinental hotel in Washington DC.

President Jakaya kikwete and the CEO of the Millennium Challenge Corporation Hon Daniel W. Johannes chat with Zanzibar’s Minister for Agriculture and Natural Resources, Mr Suleiman Othman Nyanga before a heads of state dinner hosted by Chicago Council on Global Affairs after the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Willard InterContinental hotel in Washington DC.

President Jakaya Kikwete speaks at the Centre for Strategic and International Studies (CSIS) during a Stateman’s forum on development themed “A country Transformed: A New Agenda for Tanzania”.

Tanzania’s Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives Eng. Christopher Chiza and his Zanzibar counterpart Hon Suleiman Othman Nyanga at the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete meets UK’s Secretary of State for International Cooperation Hon Andrew Mitchel in the sidelines of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.

President Jakaya Kikwete with Rock Star Bono take part in a live interview with the MSNBC television station after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. Right is NBC’s Andrea Mitchell.

US Secretary of State Hon Hillary Clinton gestures after a group photo with African leaders and the USAID Administrator Dr Rajiv Shah (third right) prior to a reception to celebrate the new partnership to advance food security on the occasion of the G-8 summit at the D. Franklin room at the State Department in Washington DC.

President Jakaya Kikwete with other leaders join US Secretary of State Hillary Clinton for a souvenir photo after the opening of the symposium themed “Food Security at the G-8: Changing the development landscape” at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.PHOTOS COURTESY OF THE STATE HOUSE.

Rais Kikwete aongoza watanzania sherehe za Muungano jijini Dar es Salaam leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia wananchi wakati alipokuwa akiingia katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam kuongoza maadhimisho ya mika 48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar leo asubuhi.

Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua vikosi vya ulinzi na usalama wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya miaka 48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mama Maria Nyerere leo katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba wakati alipowasili katika uwanja wa Uhuru kuongoza sherehe za Muungano zilizofanyika leo jijini Dar es salaam.picha na Freddy Maro.

RAIS KIKWETE MKUTANONI BRASILIA, BRAZIL,PIA ATEMBELEA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO NA UFUGAJI

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,April 17, 2012 katika mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa meza kuu na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff na wajumbe wengine katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,April 17, 2012 wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership. Kulia ni Waziri wa mambo ya Nje wa Marekani Bi Hilary Clinton.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,  April 17, 2012  kuhudhuria mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Naibu Waziri wa Masuala ya Siasa (AFRIKA) wa Brazil Balozi Paulo Cordeiro de Andrade Pinto jijini Brasilia, Brazil.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu wa Georgie Mh Nika Gilauri katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,baada ya kuhudhuria mkutano wa Open Government Partnership.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Open Government Partnership ukibadilishana mawazo kabla ya ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil. kutoka kushoto ni Waziri katika ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mh Mathias Chikawe, Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Mahadhi J. Maalim na Msahuri wa Rais (Masuala ya Siasa) Dkt Laurian Ndumbaro.

Wajumbe wa Tanzania kutoka taasisi mbalimbali za kiraia na serikali wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil,wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na mabalozi wa nchi mbalimbali wakati wa Mchapalo ulioandaliwa na Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mh Francis Malambugi nyumbani kwa Balozi usiku wa April 17, 2012 jijini Brasilia, Brazil.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akijaribu kofia aliyopewa kama zawadi na uongozi wa taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) alipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo kuhusu mashine ya kisasa ya kutambua muda wa kumwagilia maji shambani iliyoundwa na taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu ukulima wa nyanya wa kisasa katika taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA) walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu taasisi ya utafiti wa kilimo (Brazilian Agriculture Research Enterprise – EMBRAPA)walipoitembelea nje kidogo ya jiji la Brasilia.PICHA NA IKULU.

Rais Kikwete aanza ziara ya kikazi ya siku tano nchini Brazil

q

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Bw Raymond Mbilinyi, baada ya kuwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo
Mke wa Rais Mama Salma kikwete akipokea shada la maua mara baada ya yeye na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo. Kulia kwake ni Rais Kikwete na nyuma kulia ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman na mwenye miwani ni Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Mh Francis Malambugi.
Rais Jakaya Mrisho kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo. Kulia ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.
Rais Jakaya Mrisho kikwete akiongea na Msaidizi Mwandamizi wa Rais (Diplomasia) Balozi Liberata Mulamula baada ya mkutano wa maandalizi ya ziara yake ya siku tano nchini Brazil Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo. katikati ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.

Rais Jakaya Mrisho kikwete amewasili Brazil Jumapili Aprili 15, 2012 kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tano.

Katika ziara hiyo Rais Kikwete anatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Dilma Varna Rousseff wa Brazil na Rais mstasafu wa nchi hiyo Mheshimiwa Inacio da Silva Lula na viongozi waandamizi wa nchi hiyo.

Katika ziara hiyo, Rais Kikwete atahudhuria mkutano wa mwaka wa wakuu wa nchi zinazoshiriki katika Mpango wa Ubia wa Uwazi Serikalini (Open Government Partnership-OGP) utakaofanyika mjini Brasilia chini ya Uenyekiti wa Rais Rousseff na kuhudhuriwa na wajumbe wapatao mia nne (400) kutoka serikalini, Asasi zisizo za kiserikali, Sekta binafsi pamoja na Mashirika ya Kimataifa.

Ubia wa Uwazi Serikalini au kwa kifupi OGP, ni mpango uliozinduliwa Septemba 2011 mjini New York, Marekani kwa lengo la kuwapa wananchi nafasi ya kushiriki katika kuamua mambo yanayowahusu, kupitia vyama visivyo vya Kiserikali na vya Kijamii.

Ubia huu unashirikisha kwa usawa wawakilishi wa serikali kwa upande mmoja na wawakilishi wa Asasi zisizo za Kiserikali za Kijamii kwa upande mwingine. Nchi ya Brazil kwa kushirikiana na Marekani imekuwa mstari wa mbele katika kusukuma ubia huu.

Rais Kikwete anatarajiwa kuhutubia mkutano huo tarehe 17 Aprili, asubuhi mara tu baada ya hotuba ya ufunguzi itakayotolewa na Mwenyekiti wa mkutano huo Rais Dilma Rousseff wa Brazil, ambapo ataelezea maendeleo iliyofikia katika kuandaa mpango kazi wa kutekeleza ahadi ya kuongeza uwazi kama ilivyokubaliwa katika kikao kilichofanyika Disemba 2011.

Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini tarehe 20 Aprili, 2012.

RAIS KIKWETE AHANI VIFO VYA IGP STAAFU HARUN MAHUNDI NA MCHEZA SINEMA STEVE KANUMBA LEO JIJINI DAR

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,Marehemu Harun Mahundi aliyefariki Dunia april 5, 2012 na kuzikwa jana jijini Dar es salaam. Hapo ni nyumbani kwa marehemu Mikocheni barabara ya Rose Garden,jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwafariji watoto wa Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,Marehemu Harun Mahundi aliyefariki april 5, 2012 na kuzikwa jana jijini Dar es salaam.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu Steven Charles Kanumba Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo na kutoa mkono wa pole kwa wafiwa.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na waombolezaji nyumbani kwa marehemu Steven Charles Kanumba Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo alikofika kuomboleza nao msiba huo mkubwa kwa taifa letu kiujumla.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili nyumbani kwa marehemu Steven Charles Kanumba,Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo kwa ajili ya kutoa mkono wa pole kwa wafiwa,hapa akisalimianaa na mdogo wake na Marehemu Steven Kanumba.

Rais Kikwete akiwafariji wafiwa nyumbani kwa marehemu Steven Charles Kanumba Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo alikofika kuomboleza nao msiba huo.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanakamati ya msiba wa marehemu Steven Charles Kanumba Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo alikofika kuomboleza nao kifo hicho.

Rais Kikwete akiaga waombolezaji nyumbani kwa marehemu Steven Charles Kanumba Sinza ‘Vatican’ jijini Dar es salaam leo.

Rais Kikwete akiongea na waandishi wa habari wakati akiondoka msibani hapo.

RAIS KIKWETE ATOA RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA RAIS WA MALAWI HAYATI BINGU WA MUTHARIKA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Makamu wa Rais wa Malawi, Mheshimiwa Joyce Banda kuomboleza kifo cha kiongozi wa nchi hiyo, Mheshimiwa Rais Bingu wa Mutharika.

Katika salamu zake hizo, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Banda kuwa Tanzania imepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa za kifo cha Rais Bingu wa Mutharika ambaye Rais Kikwete amemwelezea kama kiongozi wa karibu na rafiki mkubwa wa Tanzania.

Amesema Rais Kikwete katika salamu hizo, “Sisi katika Tanzania tumepokea taarifa za kifo cha Rais Bingu wa Mutharika kwa mshtuko na majonzi. Alikuwa kiongozi na rafiki wa karibu wa Tanzania na rafiki yangu. Alikuwa kiongozi wa kutumainiwa miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Bara la Afrika lote.”

Ameongeza Rais Kikwete: “ Kwa hakika, Afrika imempoteza kiongozi imara, aliyeamini katika maslahi ya Bara letu na watu wake. Siku zote tutamkumbuka kwa dhamira yake na moyo wake katika kupigania umoja, amani, utulivu na ustawi wa mataifa yetu mawili na Afrika nzima.”

Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe, nakutumia wewe Mheshimiwa, familia ya marehemu na wananchi wote wa Malawi salamu za rambirambi za dhati ya mioyo yetu kufuatia kifo cha ghafla cha Mheshimiwa Rais Bingu wa Mutharika,” amesema Rais Kikwete katika salamu zake.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

 

Hayati Bingu wa Mutharika

RAIS KIKWETE KUZINDUA RASMI TUME YA KATIBA APRILI 13, 2012

Rais Jakaya Kikwete akitangaza majina ya wajumbe wa Tume ya katika

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atazindua rasmi Tume ya Kukusanya na Kuratibu Maoni ya Mabadiliko ya Katiba na kuapisha wajumbe wa Tume hiyo Ijumaa ijayo, Aprili 13, mwaka huu, 2012.

Tume hiyo itazinduliwa na wajumbe wake kuapishwa kulingana na matakwa ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 iliyounda Tume hiyo. Aidha, Tume hiyo itazinduliwa rasmi wiki moja baada ya kuwa imetangazwa rasmi. Rais Kikwete alitangaza Tume hiyo jana, Ijumaa, Aprili 6, 2012, kwenye mkutano wa wahariri uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Tume hiyo itakayoongozwa na Mwenyekiti Jaji Joseph Sinde Warioba akisaidiwa na Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu, Jaji Augustino Ramadhan ina wajumbe 30, ikiwa ni wajumbe 15 kutoka kila moja ya pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wajumbe wa Tume hiyo kutoka Tanzania Bara ni Profesa Mwesiga L Baregu, Ndugu Riziki Shahari Mngwali, Dkt. Edmund Adrian Sengodo Mvungi, Ndugu Richard Shadrack Lyimo, Ndugu John J Nkolo, Alhaji Saidi El Maamry na Ndugu Jesca Sydney Mkuchu.

Wajumbe wengine wa Tume hiyo kutoka Bara ni Profesa Palamagamba Kabudi, Ndugu Humphrey Polepole, Ndugu Yahya Msulwa, Ndugu Esther Mkwizu, Ndugu Maria Malingumu Kashonda, Mheshimiwa Al-Shaymaa J Kwegyir, Ndugu Mwantumu Jasmine Malale na Ndugu Joseph Butiku.

Wajumbe wa Tume hiyo kutoka Tanzania Visiwani ni Dkt. Salim Ahmed Salim, Ndugu Fatma Saidi Ali, Ndugu Omar Sheha Mussa, Ndugu Raya Suleiman Hamad, Ndugu Awadh Ali Saidi, Ndugu Ussi Khamis Haji na Ndugu Salma Maoulidi.

Wengine kutoka Visiwani ni Ndugu Nassor Khamis Mohammed, Ndugu Simai Mohammed Said, Ndugu Muhammed Yussuf Mshamba, Ndugu Kibibi Mwinyi Hassan, Ndugu Suleiman Omar Ali, Ndugu Salama Kombo Ahmed, Ndugu Abubakar Mohammed Ali na Ndugu Ally Abdullah Ally Saleh.

Shughuli za Tume hiyo zitaratibiwa na Sekretarieti ambayo Katibu wake atakuwa Ndugu Assaa Ahmad Rashid na Naibu Katibu atakuwa Ndugu Casmir Sumba Kyuki.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

07 Aprili, 2012

RAIS KIKWETE AOMBOLEZA KIFO CHA MWIGIZAJI NA MTAYARISHAJI FILAMU STEVEN CHARLES KANUMBA

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Steven Kanumba (enzi za uhai wake) alipokutana na wasanii wa filamu Ikulu Ndogo Dodoma mwaka jana


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania –TAFF- kuomboleza kifo cha msanii maarufu nchini Steven Charles Kanumba, aliyeaga dunia usiku wa kuamkia leo, Jumamosi, Aprili 7, 2012.

Katika salamu hizo, Rais Kikwete amemwomba kiongozi huyo wa TAFF kufikisha salamu za rambirambi za dhati ya moyo wake kwa wana-familia ya Kanumba na kwa wasaani wote nchini ambao wamepotelewa na mdau na mwenzi wao.

Rais Kikwete amesema kuwa ameshtushwa na kuzunishwa na kifo cha msanii huyo ambaye amemwelezea kuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa ambaye katika uhai wa maisha yake mafupi na akiwa bado kijana sana amechangia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya sanaa ya filamu nchini na kupitia sanaa hiyo kuitangaza Tanzania kimataifa.

Amesema Rais: ”Nimepokea kwa mshtuko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Ndugu Steven Charles Kanumba. Kupitia filamu zake, ameburudisha na kuelimisha jamii yetu kwa namna ambayo haiwezi kupimika. Alikuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa ambaye mchango wake mkubwa katika kuanzisha, kukuza na kuimarisha sanaa ya filamu nchini hautasahaulika.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Ndugu Kanumba pia ametoa mchango mkubwa katika kuitangaza nchi yetu ya Tanzania mbele ya mataifa mengine kupitia sanaa ya filamu na uwezo mkubwa wa kisanii. Tutaendelea kumkumbuka kwa mchango wake huo kwa nchi yetu.”

Nakutumia wewe Rais wa TAFF salamu zangu za rambirambi na kupitia kwako kwa wasanii wote wa filamu na sanaa nyingine kufuatia msiba huu mkubwa kwa fani yetu ya sanaa. Aidha, naomba unifikishie salamu za dhati ya moyo wangu kwa wanafamilia wote. Wajulishe kuwa niko nao katika msiba huu mkubwa. Waambie naelewa machungu yao katika kipindi hiki kigumu cha msiba,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:

Namwomba Mwenyezi Mungu awape subira na nguvu za kuweza kuhimili kipindi hiki kigumu kwa sababu yote mapenzi yake. Aidha, naungana na wana-familia na wasanii wote nchini kuwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke pema peponi roho ya Marehemu Steven Charles Kanumba. Amen.”

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

07 Aprili, 2012

Rais Kikwete akutana na na Balozi wa UAE nchini pia aagana na Balozi wa Ireland

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu(UAE) Mhe.Mallallah Mubarak Alameri ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akigana na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu(UAE) Mhe.Mallallah Mubarak Alameri baada ya kufanya naye mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Ireland anayemaliza muda wake nchini Mhe.Lorcan Fullam ikulu jijini Dar es salaam wakati balozi huyo alipokwenda kumuaga leo asubuhi.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Ireland anayemaliza muda wake nchini Mhe.Lorcan Fullam baada ya Rais kufanya naye mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.(picha na Freddy Maro)

Ujumbe wa Serikali ya Mpito ya Libya wakutana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam

Ujumbe wa Serikali ya Taifa ya Mpito ya Libya, ukiongozwa na Mheshimiwa Mahdi M Gaziri (watatu kushoto.), Mkuu wa Ofisi ya Mwenyekiti wa Serikali hiyo,ukiagana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete baada ya ujumbe huo kuwa umekutana naye Ikulu, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita (Picha na Ikulu)

Rais Kikwete akutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Unilever Global Bwana Paul Polman Ikulu jijini Dar es Salaam

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Unilever Global Bwana Paul Polman ikulu jijini Dar Es Salaam leo asubuhi.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Unilever Global Bwana Paul Polman ikulu jijini Dar es Salaam leo (picha na Freddy Maro)

President Kikwete congratulates Senegalese President Macky Sall

His Excellency Mackay Sall, President of the Republic of  Senegal

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Macky SALL, President of the Republic of Senegal, following the swearing in to the office that took place on 2nd April, 2012. The message reads as follows:

“His Excellency 

President of the Republic of Senegal

DAKAR

Your Excellency and Dear Brother,

I have received with great pleasure the news of your swearing in as the new President of the Republic of Senegal, following your landslide victory during the second run-off Presidential election that was held on 25th March, 2012.

On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania, I would like therefore to extend to Your Excellency our profound and heartfelt congratulations for being sworn into office to assume the Presidency of your great country. This is a clear testimony of the confidence reposed in you and your party by the people of the Republic of Senegal. Also, it is a clear testimony of the maturity of democracy by the people of the Republic of Senegal and thus making Senegal to be hailed as one of Africa’s model democracies.

As you embark upon your new responsibilities of that high office, I look forward to working closely with you and the Government of the Republic of Senegal to further promote the bilateral relations that so-happily exist between our two countries, for the mutual benefit of our people.

I also look forward to working closely with you in the framework of the African Union and the United Nations in our common endeavour towards achieving economic and social prosperity not only for the people of our two countries but also for the people of the continent, as a whole.

While wishing you continued good health and success in your new responsibilities, please accept, Your Excellency and Dear Brother, the assurances of my highest consideration”.


Rais Kikwete aifariji familia ya marehemu balozi Raphael lukindo leo

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu Balozi Raphael Lukindo huko Sinza jijini Dar es Salaam aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jumanne tarehe 27 Machi na kuzikwa Ijumaa tarehe 30 Machi katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dare s Salaam.Marehemu Balozi Lukindo aliyestaafu Mwaka 1988 aliitumikia serikali katika balozi mbalimbali nje ya nachi ikiwemo Japan,Urusi,Poland,Hungary na Czechoslovakia.Marehemu ameacha mjane na watoto wanne.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Bibi Tereza Mvaa Lukindo, mjane wa marehemu Balozi Raphael Lukindo wakati Rais Kikwete alipokwenda nyumbani kwa marehemu Sinza jijini Dar es Salaam kuwapa pole ndugu na jamaa kutokana na kifo cha Balozi huyo aliyezikwa juzi Ijumaa katika makaburi ya Kinondoni jijiji Dar es salaam.
Rais Kikwete akiwafariji wafiwa alipokwenda nyumbani kwa marehemu Sinza jijini Dar es Salaam kuwapa pole ndugu na jamaa kutokana na kifo cha Balozi huyo aliyezikwa juzi Ijumaa katika makaburi ya Kinondoni.
 Rais akisalimiana na watoto ndugu wa marehemu
  

RAIS Kikwete APOKEA RIPOTI YA MWAKA YA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bwana Ludovick Utouh akikabidhi ripoti yake kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Kushoto ni naibu mdhibiti n Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bwana Atanas Tarimo. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, leo, Alhamisi, Machi 29, 2012, amepokea rasmi Ripoti ya Mwaka ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kutoka kwa Mkaguzi na Mthibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bwana Ludovic Utoah kwa mujibu wa mahitaji ya Kifungu 143 (4) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika shughuli hiyo iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Rais Kikwete kwa zaidi ya saa mbili amemsikiliza Bwana Utoh akiwasilisha Ripoti hiyo ya Mwaka wa Fedha wa 2010/2011 na ambayo zamu hii imepanuliwa kwa kiasi kikubwa kulingana na mahitaji ya sasa ya ukaguzi na ikilinganishwa na ripoti za miaka iliyopita.

Bwana Utoah amewasilisha Ripoti yenye sehemu  mbili kuu ambazo ni (1) Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali Kuu na (2) Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali za Mitaa. 

Mbali na ripoti hizo mbili kuu, Bwana Utoah pia amewasilisha Ripoti ya Ukaguzi wa Mashirika ya Umma, Ripoti ya Ukaguzi wa Balozi wa Tanzania nje, Ripoti ya Miradi Mikubwa ya Maendeleo, Ripoti ya Ufanisi na Uchunguzi na Ripoti ya Ajali za Barabarani nchini.

Kwa kila ripoti, Rais Kikwete ametoa maelekezo ya usambazaji na hatimaye utekelezaji wa ripoti hizo kama ifuatavyo:

(a)          Moja, Rais Kikwete ameagiza maandalizi kufanywa na ofisi yake ili kuwasilisha rasmi Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali Kuu kwa Waziri wa Fedha na kuwasilisha Ripoti ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya ripoti hizo kuwasilishwa rasmi Bungeni ili zijadiliwe na kutolewa ushauri kama ipasavyo.

(b)         Pili, Rais Kikwete amemwelekeza Bwana Utoah kujiandaa ili aweze kuwasilisha hoja kuu zilizopo kwenye Ripoti hizo kwenye Baraza la Mawaziri ili washauri hao wakuu wa Rais waweze kujua kina nini kipo kwenye Ripoti hizo na yapi yanasemwa kuhusu Wizara mbali mbali

(c)           Tatu, Rais amemwelekeza Bwana Utoah kuhakikisha kuwa Ripoti ya Hesabu za Serikali za Mitaa inawasilishwa kwenye Mkutano Mkuu wa ALAT

(d)         Nne, Rais Kikwete amewaelekeza Mawaziri na viongozi katika ngazi mbali mbali kuzipitia Ripoti zinazohusu maeneo yao ya kazi na kuzifanyika kazi kama ipasavyo.

Rais Kikwete amemshukuru Bwana Utoah na ofisi yake kwa kazi nzuri na kumtaka kuendelea na kasi hiyo kwa sababu kazi ya kufanya bado ni kubwa.

Rais amesema kuwa amefurahi kuona ofisi ya CAG imeanza kazi ya ukaguzi wa uchunguzi na ufanisi (forensic audit) kuhusu miradi mbali mbali ya maendeleo na shughuli nyingine zinazotumia fedha za umma.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam

RAIS KIKWETE AFUNGUA WARSHA YA MIKAKATI YA KUONDOA UMASKINI LEO JIJINI DAR


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo, Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe, Balozi wa Uholanzi nchini Dkt Ad Koekkoek, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh Saidi Meck Sadick muda mfupi kabla ya kuondoka hoteli ya White Sands Hotel alikofungua warsha ya siku mbili ya Utafiti.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua warsha ya siku mbili ya mikakati ya kiuchumi ya kuondoa umaskini iliyoandaliwa na REPOA katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza  Katibu Mtendaji a Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango  akitoa mada ya ufunguzi wa warsha hiyo ya siku mbili ya REPOA. Wengine toka shoto  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe na Balozi wa Uholanzi nchini Dkt Ad Koekkoek.
Profesa Do Duc Dinh toka Vietnam akitoa mada ya jinsi nchi yake ilivyofanikiwa kuondoa umaskini warsha ya siku mbili ya utafiti juu ya mageuzi ya kuondoa umaskini nchini.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Katibu Mtendaji a Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango  kwa mada nzuri. Kati yao ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe na Balozi wa Uholanzi nchini Dkt Ad Koekkoek.
RaisDkt Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa kwa hotuba nzuri ya ufunguzi na  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa .Samuel Wangwe .
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Profesa Ibrahim Lipumba baada ya picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya siku mbili ya utafiti juu ya mageuzi ya kuondoa umaskini.Picha na Ikulu.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa moja ya magonjwa makuu yanayowakumba Watanzania kwa sasa ni ugonjwa wa Kitanzania wa kulalamika, kunung’unika wakimlaumu kila mtu isipokuwa wao wenyewe.

Aidha, Rais Kikwete amesisitiza kuwa Serikali yake itahakikisha kuwa utajiri na manufaa yanayopatikana na yatakayopatikana kutokana na raslimali za madini na gesi asilia nchini yanamnufaisha kila Mtanzania.

Rais Kikwete pia ameahidi, kwa mara nyingine tena, kuwa Serikali yake itaendelea kuwekeza katika huduma za jamii kwa kuboresha huduma za elimu na afya, kuendeleza kilimo na kuinua hali ya uchumi wa vijijini kama njia ya kuwainua Watanzania wengi zaidi, na hasa wale masikini zaidi, kutoka kwenye umasikini.

Rais Kikwete ameyasema hayo, leo, Jumatano, Machi 28, 2012, wakati alipofungua Warsha ya 17 ya Utafiti ya Mwaka ya shirika lisilokuwa la kiserikali la Research on Poverty Alleviation (REPOA) inayofanyika kwa siku mbili kwenye Hoteli ya White Sands mjini Dar es Salaam.

Rais Kikwete amewaambia washiriki wa Warsha hiyo wanaotoka nchini na nje ya nchi, na hasa wale kutoka nje ya nchi kujitahidi sana kuepukana kuambukizwa ugonjwa wa Kitanzania wa kulalamika, kunung’unika na kulaumu wakati wanapojadili changamoto na njia bora zaidi na za haraka zaidi kupunguza ama kumaliza umasikini nchini.

 “Nawaombeni nyote mlioko hapa leo kutumia nafasi ya Warsha ya Utafiti hii kwa kutathmini kwa kina kabisa changamoto zinazohujumu dhamira yetu ya kupata mageuzi ya haraka zaidi ya kiuchumi na kijamii“, amesema Rais Kikwete na kuongeza: “Mnaweza kufanya hivyo kwa kutumia ujuzi wenu wa nyuma ama kwa kutumia uzoefu wa nchi nyingine. 

Tafadhalini sana epukeni  na jizuieni sana kutokuambukizwa ugonjwa wa Kitanzania wa kulalamika na kulaumu wengine wote isipokuwa sisi wenyewe. Ni ugonjwa usiokuwa na tija.”

Kuhusu nafasi ya raslimali za madini na gesi asilia nyingi iliyogunduliwa nchini, Rais Kikwete amerudia tena ahadi yake ambayo ameitoa huko nyuma kuwa Serikali yake itahakikisha kuwa raslimali hizo zinawanufaisha Watanzania wote bila kubagua kwa sababu kila Mtanzania anayo haki ya kunufaika na raslimali za nchi yake.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete ambaye amesisitiza mageuzi makubwa ya sera ambako sasa wajibu wa Serikali ni kufungua njia za uwezeshaji na sekta binafsi kufanya biashara tofauti na sera za zamani ambako Serikali ilikuwa inafanya hata biashara ya bucha za nyama na maduka ya sindano na viberiti amewaambia washiriki wa Warsha hiyo:

“Serikali kwa upande wake itaendelea kutekeleza mipango na sera ambazo zinamnufaisha kila mtu na zenye kuhudumia maslahi ya jamii zilizo masikini zaidi na zisizojiweza. Tutaendelea pia, kuwekeza zaidi katika huduma za jamii kwa kuinua kiwango na ubora wa elimu, huduma za afya, kuboresha kilimo na uchumi wa maeneo ya vijijini.”

Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
28 Machi, 2012

RAIS KIKWETE AONGOZA MAZISHI YA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA LIWALE HAYATI VICTOR PAUL CHIWILE LEO KIBAHA

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za Mwisho kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Liwale Marehemu Victor Paul Chiwile wakati wa mazishi Kibaha Picha ya Ndege mkoa wa Pwani leo.

Rais Jakaya Kikwete akiweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Liwale Marehemu Victor Paul Chiwile wakati wa mazishi Kibaha Picha ya Ndege mkoa wa Pwani leo.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilal, Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh Mwantumu Mahiza na Mkuu wa Mkoa wa Lindi wakiwa mazikoni.PICHA NA IKULU.

Rais Kikwete awaapisha Makatikbu Tawala wa Mikoa ikulu jijini Dar Es Salaam

Katibu Tawala mpya wa mkoa wa Mbeya Bibi.Mariam Mtunguja akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es salaam leo.Katika hafla hiyo Rais aliwaapisha pia makatibu Tawala wa mikoa mingine kama ifuatavyo,Dkt. Faisal Issa (Kilimanjaro),Bwana Eliya Ntandu (Morogoro), Bwana Severine Kahitwa (Geita),Bwana Emmanuel Kalobelo (Katavi), Bwana Hassan Bendeyeko (Ruvuma) na Dkt. Anselem Tarimo (Shinyanga).(Picha na Freddy Maro).

RAIS KIKWETE AZUNGUMZA NA NAIBU WAZIRI WA BIASHARA WA CHINA IKULU LEO


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na  Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao  na ujumbe wake walipomtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo. Mawaziri wa Fedha Mh Mustafa Mkullo, Uchukuzi Dr Omar Nundu na Nishati na Madini Mh William Ngeleja walihudhuria mazungumzo hayo.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kumtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kumtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo. Katikati yao ni mkalimani na wengine ni ujumbe wa Mh Jonzhao.PICHA NA IKULU.

Rais Kikwete azindua mradi wa maji Pawaga, mkoani Iringa

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizindua mradi wa maji katika kijiji cha Itunundu,Pawaga wilaya ya Iringa vijijini leo.Wapili kushoto ni Askofu wa Kanisa la Kianglikana Dayosisi ya Ruaha Dr. Joseph Ng’habi na wanne kushoto ni Askofu Mstaafu Donald Mtetemela.Mradi huo umefadhiliwa na Dayosis ya Ruaha Kanisa la Anglikana na marafiki zao.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akikagua chanzo cha maji katika kijiji cha Pawaga kilichopo wilaya ya Iringa vijijini. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu

Rais Kikwete awaapisha wakuu wa mikoa mipya ya njombe, simiyu, katavi na geita leo

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Kapt Asery Msangi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe katika sherehe zilizofanyika leo asubuhi Ikulu jijini Dar es salaam

 Rais akimwapisha Kapt. Paschal Kulwa Mabiti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu

 Rais Kikwete akimwapisha Mh Magalula Saidi Magalula kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita

 

Rais Kikwete akimwapisha Dkt Rajab Mtumwa Rutengwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Rais Kikwete amuapisha Mkuu Mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba ikulu Jijini Dar es Salaam

Amiri Jeshi mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(Katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange(kushoto) na Mkuu mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo(picha na Freddy Maro).
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,(kushoto)Waziri Mkuu Mizengo Pinda(kulia) na Mkuu mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha mkuu huyo mpya wa JKT ikulu jijini Dar es Salaam leo.
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mzee Albert Ndomba(85),baba mzazi wa Mkuu Mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba(wapili kushoto) baada ya halfa ya kumuapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni mke wa Meja Jenerali Ndomba na waliosimama nyuma ni wanafamilia.
Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi mkuu mpya wa JKT meja Jenerali Samwel Ndomba wakati wa hafla ya kumuapisha iliyofanyika leo asubuhi ikulu jijini Dar es Salaam.

Mkuu Mpya wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) Meja Jenerali Samwel Ndomba akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Meja Jenerali Ndomba anachukua nafasi ya Meja Jenerali Samwel Kitundu aliyestaafu hivi karibuni kwa mujibu wa sheria.

RAIS KIKWETE AOMBOLEZA KIFO CHA MWAKILISHI WA BUBUBU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho kuomboleza kifo cha Mwakilishi wa Jimbo la Bububu (CCM) Mheshimiwa Salum Amour Mtondoo.

Hayati Mtondoo alizikwa kijijini kwao Bumbwini, Mkoa wa Kaskazini Unguja jana, Ijumaa, Machi 16, 2012, baada ya kufariki dunia juzi kwa matatizo ya shinikizo la damu, malaria na sukari.

Katika salamu zake kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, Rais Kikwete amesema kuwa amepokea kwa mshtuko na masikitiko habari za kifo cha Mheshimiwa Mtondoo ambaye alikuwa Mwakilishi wa Wananchi wa Bububu katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi.

“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko habari za kifo cha Mheshimiwa Mtondoo. Siyo tu alikuwa mwanachama hodari wa chama chetu, lakini pia katika kipindi chake cha uwakilishi amefanya kazi nzuri na ya kukumbukwa ya kutetea ipasavyo maslahi ya wananchi wa jimbo lake kwa uadilifu na moyo mkubwa wa kujituma,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:

“Kupitia kwako Mheshimiwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, natuma salamu za dhati ya moyo wangu kwa Wawakilishi wote kwa kuondokewa na wenzao, kwa wananchi wa Bububu kwa kumpoteza mwakilishi wao hodari na kwa wana-CCM wa jimbo hilo kwa kifo cha mwanachama mwenzetu.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Aidha, naomba uniwasilishie salamu zangu kwa wanafamilia wote wa Mheshimiwa Mtondoo kwa kupotelewa na mhimili mkuu wa familia. Wajulishe kuwa niko nao katika msiba huu mkubwa. Aidha, nawaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, awape subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu. Amen.”

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

17 Machi, 2012

Rais Kikwete ateua wakuu wa mikoa wa katavi, Geita, simiyu na Njombe

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABAR

          Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wafuatao kuwa Wakuu wa Mikoa.

          Dkt. Rajab Mtumwa RUTENGWE ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa KATAVI.  Kabla ya hapo Dkt. Rutengwe alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda.

Ndugu Magalula Saidi MAGALULA ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa GEITA.  Kabla ya hapo Ndugu MAGALULA alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi.

          Ndugu Paschal Kulwa MABITI ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa SIMIYU.  Kabla ya hapo Ndugu MABITI alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida.

Kapt. Asery MSANGI ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa NJOMBE.  Kabla ya hapo Kapt. MSANGI alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa.

Uteuzi huu unaanza tarehe 15 Machi, 2012.  Wataapishwa Ikulu, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 21 Machi, 2012 saa 04:00 asubuhi.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

15 Machi, 2012

Rais Kikwete afungua warsha ya chama cha madaktari wa Kinywa na Meno leo jijini Dar

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mkutano wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma. Jumla wa wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo wa siku tatu unaofanyika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati Rais wa chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Nchini Dk. Rachel Mhavile akionesha kadi ya uanachama wa heshima ya chama hicho ambayo Rais Kikwete akitunukiwa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma. Jumla wa wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo wa siku tatu unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea tuzo maalumu toka ka Rais wa chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Nchini Dk. Rachel Mhavile wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma. Jumla wa wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo wa siku tatu unaofanyika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma jarida la Meno Tanzania alilokabidhiwa na Rais wa chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Dk. Rachel Mhavile mara baada ya kufungua mkutano wa siku tatu wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma . Jumla ya wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wajumbe wanahudhuria mkutano wa siku tatu wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma wakimsikiliza Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano huo. Jumla ya wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais wa chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Nchini Dk. Rachel Mhavile (kulia) na Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dk. Donnan Mmbando baada ya kufungua mkutano wa siku tatu wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma ambapo jumla ya wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo.

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano wa siku tatu wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akagua mradi wa umwagiliaji Msoga

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua chanzo cha maji katika mradi wa umwagiliaji maji katika kijiji cha Msoga,wilayani Bagamoyo, mkoa wa Pwani leo mchana.Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Pwani Bi.Mwantumu Mahiza na kushoto ni mwenyekiti wa kijiji cha Msoga Bwana Herman Katoto Semindu.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mkulima Selemani Ramadhani katika shamba la kijiji lililopo katika mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Msoga kilichopo wilayani Bagamoyo leo asubuhi wakati alipotembelea kukagua maendeleo ya mradi.Jumla ya hekta mia nne zimetengwa kwa ajili ya mradi huo.(picha na Freddy Maro)

Mabalozi wa Vatican, Saudia na Zambia wawasilkisha hati zao kwa Rais Dkt.Jakaya Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea hati za utamblisho kutoka kwa mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania.Waliowasilisha hati zao leo ikulu jijini Dar es Salaam ni pamoja na Mhe. Hani Bin Abdullah bin Mohamed Mu’minah wa Saudi Arabia, Askofu Mkuu Mhashamu Francisco Mentecillo Padilla wa Vatican, na Mhe.Bi. Judith Kangoma Kapijimpanga wa Zambia.Pichani Balozi mpya wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Mhashamu Francisco Montecillo Padilla akiwasilisha hati zake kwa Rais Kikwete.Katikati anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Antony Itatiro.(picha na Freddy Maro).

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, leo Alhamisi, Machi 8, 2012, amepokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wa nchi tatu ambao wataziwakilisha nchi zao katika Tanzania.

Katika sherehe fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete amepokea hati za Balozi Hani Abdullah Mominah wa Saudi Arabia, Askofu Mkuu Francisco Montecillo Padilla wa Vatican na Mheshimiwa Judith Kangoma-Kapijimpanga wa Zambia.

Katika mazungumzo mafupi baada ya kuwa amewasilisha hati zake za utambulisho, Rais Kikwete amemwambia balozi mpya kuwa baada ya Tanzania na Saudia Arabia kufanikiwa kujenga uhusiano wa karibu katika nyanja za kisiasa na kidiplomasia, sasa ni wakati wa kuimarisha uhusiano wa kiuchumi.

Katika mazungumzo yake na Rais Kikwete, Balozi Padilla amemwasilishia Rais ujumbe wa Baba Mtakatifu Benedict wa 16 ambako kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani amesifu amani, haki, umoja na mshikamano uliojengeka miongoni mwa Watanzania tokea uhuru mwaka 1961.

Rais Kikwete ameshukuru kupokea pongezi na sifa hizo za Baba Mtakatifu na kuongeza kuwa pamoja na majaribio yote bado Tanzania imeendelea kuwa nchi yenye umoja, amani na mshikamano pamoja na kwamba ina makabila mengi, tamaduni tofauti, watu wa rangi mbali mbali na tofauti na imani mbali mbali.

“Yetu ni nchi inayoishi katika amani na mshikamano pamoja na kuwepo kwa tofauti nyingi za makabila, za dini na imani, za tamaduni tofauti “, Rais Kikwete amemwambia Balozi Padilla.

Rais na Kikwete na Balozi Kapijimpanga wa Zambia wamezungumzia hali ya uhusiano nzuri uliopo kati ya nchi hizo mbili na jinsi gani ya kuimarisha zaidi uhusiano huo na jinsi ya kuendelea kushirikiana katika uendeshaji wa miradi ya pamoja.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

08 Machi, 2012

President Kikwete launches Country Review Mission for APRM

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with members of African Peer Review Mechanism(APRM) group of experts at Dar es Salaam State House this morning.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete presents the Tanzania Country Assessment Report to an APRM (Africa Peer Review Mechanism) Lead Panelist Barrister Mr. Akere Muna. during a function held at State House Gardens in Dar es Salaam, this morning.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, The Vice President Dr.Mohamed Gharib Bilal(third left) and Prime Minister Mizengo Pinda(third right) in a group picture with members of African Peer Review Mechanism (APRM ) group of experts shortly after he presented a Tanzania Country Review Report and launched the country’s Review Mission at State House Dar es Salaam this morning.Photos by Freddy Maro.

RAIS KIKWETE AFUNGAU MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI LEO MJINI MOSHI

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Chuo cha Polisi mjini Moshi leo tayari kwa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani,Mh. Shamsi Vuai Nahodha na kushoto kwake ni Inspekta Jenerali wa Polisi,Saidi Mwema.

Rais Dkt. Jakaya Kikwete akizindua mojawapo ya vitabu vya muongozo wa Jeshi la Polisi wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Chuo cha Polisi mjini Moshi leo.Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani,Mh. Shamsi Vuai Nahodha wa kulia kwa Rais ni Inspekta Jenerali wa Polisi,Saidi Mwema akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Mh. Leonidas Gama.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Chuo cha Polisi mjini Moshi leo.

Sehemu ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Chuo cha Polisi uliofunguliwa na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mjini Moshi leo.PICHA NA IKULU

 

HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI WA KUFUNGUA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI,

CHUO CHA POLISI MOSHI, TAREHE 06 MACHI 2012

Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi;

Inspekta Generali wa Polisi, Said Ally Mwema;

Mheshimiwa Leonidas Gama, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro;

Makamishna na Manaibu Makamishna wa Jeshi la Polisi;

Maofisa Wakuu wa Jeshi la Polisi;

Wageni waalikwa;

Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana wewe Mheshimiwa Waziri pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini kwa kunialika kuja kufungua Mkutano wenu. Nakupongeza kwa dhati Mkuu wa Jeshi la Polisi na viongozi wenzako kwa kuwa na utaratibu wa kukutana kila mwaka kufanya tathmini ya shughuli zenu. Huu ni utaratibu mzuri kwa vile kila Kamanda kwa ngazi yake anatoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa sera, mikakati na mipango mbalimbali ihusuyo usalama wa raia na mali zao katika eneo lake la uongozi.

Nathubutu kusema kuwa msingeweza kuwa na utaratibu mwingine mzuri kushinda huu. Matumaini yangu ni kuwa taarifa hizo zinafanya uchambuzi wa kina wa mafanikio yaliyopatikana, kasoro zilizojitokeza na changamoto mlizokabiliana nazo na mnazoendelea kukabiliana nazo. Aidha, ni matumaini yangu kuwa mjadala unakuwa wa uwazi na ukweli na kwamba hamtaoneana muhali kuambiana ukweli kuhusu kasoro za mwenzenu pale inapostahili. Ni jambo jema na la kijasiri kujiwekea utaratibu wa kujipima wenyewe.

Mheshimiwa Waziri,

Ndugu Mkuu wa Jeshi la Polisi;

Nimefurahishwa sana na Kauli Mbiu ya mkutano wenu “Usingoje, tumia rasilimali ulizonazo kuongeza ufanisi”. Ni Kauli Mbiu muafaka inayohimiza uwajibikaji na ufanisi wa kazi kwa kuzingatia rasilimali zilizopo. Inatambua hali halisi kwamba utegemee ulichonacho kutimiza majukumu yako. Usisubiri usichokuwa nacho. Usisubiri ulichoomba au ulichoahidiwa kupata. Nawaomba mkitoka hapa mwende kwenye vituo vyenu vya kazi mkiwa mmebeba ujumbe huu mzito wa Kauli Mbiu. Mwende mkatekeleze maudhui yake kwa vitendo, kwa kushirikiana na maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali. Mkifanya hivi, bila shaka mtaweza kukidhi matarajio ya wananchi na hivyo kulinda heshima ya Jeshi letu la Polisi.

Ni ukweli ulio wazi kuwa sote tungetamani muwe na zana na vitendea kazi vilivyo bora, vingi vya kutosheleza mahitaji yetu. Lakini uwezo wa kifedha uliopo ni mdogo, vitu hivyo unavyovitaka hutavipata vyote kwa wakati mmoj. Hivyo basi hamna budi kuwa na subira, kupanga vipaumbele vyenu vizuri na hasa kuwa wabunifu ili kwa kutumia vifaa vilivyopo vizuri muweze kutekeleza majukumu yenu kwa kiwango cha kuridhisha.

Mheshimiwa Waziri;

Ndugu IGP,

Maafisa na Askari,

Nataka kuwahakikishia kuwa mimi na viongozi wenzangu Serikalini tunatambua umuhimu wa kuendelea kuliongezea Jeshi la Polisi uwezo wa kibajeti ili liweze kutimiza kwa ufanisi zaidi majukumu yake. IGP ni shahidi kwa kiasi gani tumeendelea kuongeza bajeti ya Jeshi la Polisi mwaka hadi mwaka. Kwa mfano, mwaka 2005 Bajeti ilikuwa Shilingi 69 bilioni na mwaka huu wa fedha zimetengwa Shilingi 134 bilioni. Nawaahidi kuwa tutaendelea kuongeza fedha kila mwaka katika miaka ijayo. Pia tumetumia uhusiano wetu na nchi rafiki kuomba misaada inayoendelea kuimarisha Jeshi letu kwa zana, mafunzo na weledi.

Napenda kutumia nafasi hii kuwapongeza Maofisa, Wakaguzi na askari wote kwa kazi kubwa na nzuri muifanyayo katika kulinda maisha na mali za raia. Nawapongeza kwa uchapakazi wenu na moyo wenu wa kujitolea na kujituma. Hakika maudhui ya Kauli Mbiu yenu ya mwaka huu mmekuwa mnayatekeleza kwa vitendo. Matokeo ya jitihada zenu yanaonekana. Mafanikio ya kutia moyo yanazidi kupatikana na sote tunayashuhudia. Mwenye macho haambiwi tazama. Uhalifu (hususan wa kutumia nguvu) unaendelea kupungua nchini kuliko ilivyokuwa miaka ya nyuma. Kulingana na takwimu za mwaka wa jana makosa makubwa ya jinai yalipungua kutoka 94,390 mwaka 2010 hadi 76,052 mwaka 2011.

Haya ni mafanikio ya kutia moyo, lakini hamna budi mtambue kuwa bado idadi ya makosa 76,052 ni kubwa mno. Hivyo bado mnayo na tunayo kazi kubwa ya kufanya mbele yenu na yetu. Inatupasa tuongeze juhudi maradufu au hata zaidi ili tupunguze kabisa uhalifu nchini.

Ndugu Makamanda,

Maofisa Waandamizi wa Polisi;

Mheshimiwa Waziri na Inspekta Generali wamezieleza vizuri changamoto zinazolikabili Jeshi la Polisi na mimi sina haja ya kuzirudia. Napenda kutumia nafasi hii kurudia kuwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kusaidiana nanyi kwa kuwawezesha ili muweze kuzikabili changamoto hizo kwa mafanikio. Tumefanya hivyo miaka iliyopita, tunafanya hivyo hivi sasa na tutafanya hivyo miaka ijayo.

Tutaendelea kuliwezesha Jeshi la Polisi kifedha ili muweze kutekeleza ipasavyo majukumu yenu. Tutaendelea kuwawezesha muongeze idadi ya askari. Tutawawezesha mpate vyombo vya usafiri, zana na vitendea kazi vya kisasa vya kufanyia kazi za kukabiliana na uhalifu. Kazi ya kulipatia Jeshi la Polisi zana na vifaa vipya vya kazi inaendelea ikiwa ni sehemu ya Programu ya Maboresho ya Jeshi la Polisi. Nawahakikishia kuwa tutaendelea kutoa fedha za kutekeleza Programu hiyo na shughuli nyingine za Jeshi la Polisi.

Tutaendelea kuwawezesha katika kuboresha mafunzo ya askari na maafisa wa Jeshi la Polisi. Natambua mahitaji ya kuviboresha vyuo vilivyopo sasa. Panapohitaji kukarabati pakarabatiwe na panapotakiwa ujenzi wa majengo mapya yajengwe. Na panapotakiwa kuanzishwa chuo kipya kianzishwe. Hatuna budi kuwekeza katika mafunzo kwani mafunzo ni msingi mzuri wa weledi na kuwa na askari wenye tabia na mwenendo mwema. Kupata zana za kisasa za upelelezi na kudhibiti uhalifu pekee hazitoshi kama zitakuwa mikononi mwa askari asiyejua kitu, asiyekuwa na nidhamu na utiifu. Kufanya hivyo kunalihakikishia Jeshi uwezo wa kutimiza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa na kuleta sifa kwa Jeshi la Polisi Tanzania.

Dunia imebadilika, Tanzania imebadilika na mbinu za uhalifu na aina za uhalifu yamebadilika. Pia, mbinu, mikakati na maarifa ya kukabiliana na uhalifu, nayo yamebadilika duniani. Lazima tusisitize mafunzo, kwani ndiyo msingi wa weledi na ufanisi. Mafunzo ndiyo njia ya kuwawezesha askari na maofisa wa Jeshi la Polisi kupata elimu na maarifa mapya kuhusu uhalifu na namna ya kukabiliana nao. Mafunzo ndiyo yatakayowezesha kuelewa zana na vifaa vipya vya kupambana na uhalifu na kujua namna ya kuvitumia. Hakuna badala ya mafunzo.

Mheshimiwa Waziri,

Ndugu Inspekta Jenerali,

Maofisa,

Wakaguzi na Askari;

Mimi na wenzangu katika Serikali tunatambua umuhimu wa kuboresha maslahi ya maofisa na askari wa Jeshi la Polisi pamoja na kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kuishi. Mara baada ya kuchaguliwa mwaka 2005, nilipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na baadhi ya kambi nilijifunza mengi kuhusu hali ya maslahi na mazingira ya kazi na malazi ya wanajeshi wetu. Baada ya hapo tulianza kuyachukulia hatua mambo hayo na tumekuwa tunaendelea kufanya hivyo hadi sasa. Tumeboresha maslahi kwa kiasi chake na bado tunaendelea. Tumeanza ujenzi wa nyumba bora za kuishi na bado tunaendelea na mpango huo.

Napenda kurudia kuwahakikishia kuwa kwangu na wenzangu Serikalini, hakuna upungufu wa dhamira ya kuboresha na kuimarisha Jeshi la Polisi nchini kwa maana ya idadi, mafunzo, vitendea kazi, maslahi na mazingira ya kuishi. Kinachotutatiza ni uwezo wa kifedha wa Serikali ambao si mkubwa sana kuweza kumudu sawia mahitaji yote ya kugharamia shughuli zote za Serikali na Taifa. Pamoja na changamoto hizo, bado tumeendela kuthubutu kuchukua hatua na kwa haya tuliyoweza kufanya kwa upande wa Jeshi la Polisi si haba. Tunaendelea.

Mheshimiwa Waziri,

Ndugu IGP;

Sina budi kuelezea furaha yangu na pongezi za dhati kwako IGP, Makamishna walioko Makao Makuu ya Polisi pamoja na Makamanda wa ngazi mbalimbali kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana kutokana na rasilimali iliyopo. Huu ni uthibitisho wa uongozi wako makini ukishirikiana na viongozi wa ngazi mbalimbali wa Jeshi letu. Hakika Kauli Mbiu ya mwaka huu kwenu si jambo geni hivyo tunategemea kuona mafanikio makubwa zaidi miaka ijayo. Aidha, mnanipa moyo kuwa hapo rasilimali zitakapoongezeka Jeshi la Polisi litastawi sana.

Usalama Barabarani

Mheshimiwa Waziri,

Inspekta Generali wa Polisi,

Ndugu Makamanda;

Napenda kutumia nafasi hii kurudia maombi yangu kwenu kuimarisha usimamizi wa usalama barabarani. Ajali za barabarani zimezidi mno, hatuna budi kuzizuia zisizidi kuongezeka. Tufanye kila tuwezalo zipungue. Nawaomba mtumie fursa ya mkutano wenu huu kujadili tatizo hili kwa marefu na mapana yake na mkubaliane juu ya nini cha kufanya. Naamini mtaweza.

Nawaomba jambo hili mlipe uzito unaostahili kabla halijageuka kuwa janga la kitaifa. Ukweli kwamba katika kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka juzi (2010) jumla ya watu 3,687 walipoteza maisha kutokana na ajali za barabarani. Mwaka na jana (2011) katika kipindi hicho hicho idadi hiyo iliongezeka na kufikia watu 4,013. Hili si ongezeko dogo inatulazimu kushtuka na kuchukua hatua. Nafahamu dhana ya kuwianisha kuongezeka kwa ajali na kuongezeka kwa pikipiki na magari na hali ya barabara zetu. Hata hivyo hivi visiwe visingizio vya kuona kuongezeka kwa ajali za barabarani ni jambo la kawaida. Tuseme ukweli kuwa ajali nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva kutokuheshimu Sheria ya Usalama Barabarani na ubovu wa vyombo vya usafiri. Kwa sababu zote hizi mbili Jeshi la Polisi lina wajibu maalum kukabiliana nazo. Tafadhali timizeni ipasavyo wajibu wenu. Mkajipange vizuri, kwa kushirikiana na Idara nyingine husika za Serikali, ili ajali na vifo viweze kupungua.

Madereva wazembe, walevi na wasiotaka kufuata Sheria na Kanuni za usalama barabarani wachukuliwe hatua kali. Wakati umefika madereva wakaidi wanyang’anywe leseni zao ili wasihatarishe tena maisha ya Watanzania. Najua haiwezekani kukomesha kabisa ajali za barabarani, lakini naamini kuzipunguza inawezekana. Endapo kuna msaada mnahitaji au jambo mnataka kutoka kwetu, tuambieni. Kama mnadhani Sheria ya Usalama Barabarani na Kanuni zake zinahitaji marekebisho, tuleteeni mapendekezo yenu tuyafanyie kazi. Au kama mnaona kuna mapungufu katika mfumo wa kitaasisi uliopo, msisite kutushauri na sisi tutaangalia namna ya kurekebisha.

Mheshimiwa Waziri,

Ndugu IGP,

Makamanda, Maafisa na Askari,

Jambo lingine ninalopenda mlizungumze kwa kina na mkubaliane katika Jeshi letu ni juu ya hatua za kuchukua dhidi ya tuhuma za kuenea kwa vitendo vya rushwa katika Jeshi la Polisi. Najua mnajitahidi lakini bado ni hisia ya muda mrefu ya wananchi na haionekani kubadilika. Utafiti unaofanywa na taasisi zinazojihusisha na masuala ya utawala bora kuhusu rushwa bado zinalinyooshea kidole chombo chetu hiki muhimu sana cha dola. Natamani sana hisia na taarifa hizo ingekuwa hazina chembe ya ukweli lakini, bahati mbaya huo ndio mtazamo wa jamii na inaelezea wakati mwingine kwa nini baadhi ya wananchi huchukua sheria mikononi mwao.

Pamoja na kuwepo kwa hisia hizo mimi naamini wapo Polisi wengi wazuri na kwamba hali haijafikia kusema imeshindikana kupambana na kukomesha vitendo vya rushwa katika Jeshi la Polisi. Penye nia pana njia. Tafadhali sana tieni nia ya dhati kupambana na tatizo hili na kushinda. Watambueni wale wenzenu miongoni mwenu wenye tabia ya kuomba kitu kidogo muwawajibishe ipasavyo kwa adhabu zinazostahili. Hawa ni watu wanaosaidia wahalifu wasibanwe na mkono wa sheria hivyo ni kikwazo kwa Jeshi la Polisi kutimiza ipasavyo wajibu wake wa msingi wa kupambana na uhalifu. Waondoeni katika Jeshi kwani wanaharibu sifa yenu nzuri na kudhoofisha Chombo chetu.

Mheshimiwa Waziri,

Ndugu IGP,

Ndugu Makamishna,

Maofisa Waandamizi wa Polisi;

Mabibi na Mabwana;

Yamekuwapo malalamiko mengi ya ukiukwaji wa haki za binadamu yanayoelekezwa kwa Jeshi letu la Polisi katika utendaji kazi. Taarifa za kila mwaka zinazotolewa na Tume ya Haki za Binadamu na taasisi nyingine mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa zimekuwa zikionesha hivyo. Yapo pia madai ya watu kunyanyaswa na Polisi kwa kukamatwa bila makosa, kubambikiwa makosa, kuteswa wakiwa mahabusu na hata kuuliwa. Kuna madai ya Polisi kutumia nguvu kupita kiasi na hata kusababisha vifo ya raia.

Nawaomba mtumie fursa ya mkutano huu myazungumze madai hayo na kuamua hatua zipasazo za kuchukua. Natambua kuwa katika Programu ya Maboresho ya Jeshi kuwaelimisha wanajeshi wetu kuhusu masuala ya haki za binadamu ni moja ya mambo yaliyopewa kipaumbele. Nawaomba mtekeleze dhamira yenu hii njema kwa kasi zaidi ili katika kipindi kifupi muwafikie Polisi wetu wote. Aidha, mafunzo kuhusu haki za binadamu yawemo katika mitaala ya vyuo vyetu hapa CCP, Police College – Kurasini na Chuo cha Maafisa Wakuu Kidatu.

Aidha, Jeshi liweke utaratibu mzuri na unaoeleweka wa kupokea na kufanyia kazi malalamiko au maoni yanayopelekwa kwao na wananchi.

Ni muhimu kwa Jeshi la Polisi kusisitiza na kusimamia kwa dhati nidhamu ya maofisa na askari wake. Nidhamu ni sifa ya msingi ya askari. Askari asiye na nidhamu amepoteza sifa ya kuendelea kuwa mwanajeshi. Ni hatari sana kwa usalama wa raia na anaharibu sifa ya Jeshi. Vitendo vya utovu wa nidhamu vinavyofanywa na baadhi ya maofisa na askari kamwe visivumiliwe. Hivi majuzi nimesikia kuwa hapa Moshi askari ametoroka lindo na kwenda disco, tena akiwa na silaha! Vitendo vya namna hii vinaleta fedheha kwa Jeshi la Polisi na kuwaacha watu wakishangaa na kuwa na maswali mengi juu ya Jeshi lao. Inawezekanaje ifikie hapo kwa askari aliyefunzwa vizuri.

Nawaomba mzingatie upya taratibu zenu za ajira. Wakati umefika wa kuwepo na utaratibu mzuri wa upekuzi wa vijana kabla ya kuteuliwa kusomea kazi ya Polisi. Pawepo na utaratibu thabiti na kufuatilia mienendo ya askari wakati wote wa utumishi wao. Majeshi mengine yanafanya hivyo. Kufanya hivyo kutasaidia kupata vijana walio safi kwa tabia na mwenendo kuajiriwa na kuendelea na utumishi katika Jeshi la Polisi. Kwa ajili hiyo tutakuwa na askari walio watiifu, waaminifu, wachapa kazi hodari na kuliletea sifa Jeshi letu.

Mwisho

Mheshimiwa Waziri,

Inspekta Generali,

Makamanda wa Polisi;

Kabla ya kumaliza hotuba yangu napenda kurudia kutoa pongezi za dhati kwa kazi kubwa na nzuri muifanyayo pamoja na changamoto mbalimbali mnazokabiliana nazo. Nawapongeza sana kwa kubuni utaratibu wa Polisi Jamii ambao ni mfano mzuri wa ubunifu wa kutumia rasilimali zilizopo. Tafadhali uimarisheni na kuuboresha utaratibu huu mzuri. Sisi katika Serikali tutafanya kila linalowezekana kuongeza rasilimali kwa Jeshi la Polisi ili kuliwezesha kukabiliana na uhalifu nchini. Nawaomba mkumbuke na kuzingatia ukweli kwamba katika kila hatua mnayopiga, sisi Serikalini na taifa zima kwa ujumla tutakuwa pamoja nanyi kuwapa moyo na kuwaunga mkono kwa rasilimali muhimu.

Ndugu Inspekta Jenerali,

Makamanda wa Mikoa na Vikosi,

Mabibi na Mabwana,

Baada ya kusema hayo, ninayo furaha sasa kutamka kwamba, Mkutano Mkuu wa Mwaka 2012 wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi umefunguliwa rasmi. Nawatakia mkutano mwema, mazungumzo yenye ufanisi na matokeo mazuri.

“Ahsanteni kwa kunisikiliza”

President Kikwete launches campaign against cruelty and violence against women

President Jakaya Mrisho Kikwete with the Minister for Community Development Gender and Children, Sophia M. Simba, Assistant Secretary General of the United Nations, Mr. John Hendra, First Lady Mama Salma Kikwete and the Regional Commissioner of Kilimanjaro Region Leonidas Gama join 90 gallant men and women from 36 African countries who are climbing Mt. Kilimanjaro with the objective of drawing attention to the important issue of fighting violence against women and girls.

President Jakaya Mrisho Kikwete with the Minister for Community Development Gender and Children, Sophia M. Simba, Assistant Secretary General of the United Nations, Mr. John Hendra,flag off the climb.

President Jakaya Mrisho Kikwete speaks at the launch of the climb at the Kilimanjaro National Parks Marangu gate.

President Jakaya Mrisho Kikwete presents General Mirisho Sam Hagai Sarakikya, the country’s top climber who at 78 years of age has scaled to the roof of Africa 38 times and plans to make his final climb when he turns 80.

President Jakaya Mrisho Kikwete with young climbers from Botswana.PHOTOS BY STATE HOUSE

OPENING SPEECH BY HIS EXCELLENCY DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DURING THE FLAGGING OFF CEREMONY FOR “CLIMB UP –SPEAK OUT” MOUNT KILIMANJARO CLIMB TO END VIOLENCE AGAINST WOMEN AND GIRLS ON 5TH MARCH, 2012

AT MARANGU, KILIMANJARO REGION, TANZANIA

Honorable Minister for Community Development Gender and Children, Sophia M. Simba (MP);

Mr. John Hendra, Assistant Secretary General of the United Nations;

Leonidas Gama, Regional Commissioner of Kilimanjaro Region

Members of the Diplomatic Corps Present;

All Climbers; Distinguished Guests, Ladies and Gentlemen;

Introduction

I thank you Honourable Minister for your kind invitation and for affording me this rare privilege to see off 90 gallant men and women from 36 African countries who are climbing Mt. Kilimanjaro with the objective of drawing attention to the important issue of fighting violence against women and girls. I welcome you all to Marangu and for those who come from outside Tanzania welcome to your other home away from home. I wish you a successful climb and I pray that all of you will reach the summit and feel the sense of conquest and accomplishment when you are on roof of Africa.

On behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania, I thank the organisers for availing our country, this great honour of hosting this memorable event, the Africa UNITE Climb to End Violence against Women and Girls which will start shortly. Allow me also to take this opportunity to commend the United Nations’ Secretary General, H.E. Ban Ki-Moon for conceiving the Africa UNiTE Campaign. Tanzania strongly supports the Secretary General’s Campaign on “Say No – UNiTE to End Violence against Women and Girls”.

The fact that 36 African countries are represented at this event today signifies Africa’s commitment to ending violence against women and girls in our continent. I was personally pleased to launch the Tanzanian chapter of this Campaign on the 24th May 2008. I am even comforted to see that the campaign has taken a life of its own in Africa and is indeed highlighting in unprecedented ways the problem of gender based violence.

Impact of Violence against Women

Your Excellencies, Ladies and Gentlemen;

Violence against women is pervasive scourge which has been with us for ages. It knows no color, creed, age, status or nation. It’s in every country. What brought us here is the fact that we should not allow this cruel and worthless scourge to continue. Now is the time to intensify efforts to fight it. It does no good to women other than pain and suffering both physically and emotionally. It is a violation of women’s rights of a very high degree. It demeans their personality and humanity.

It prevents women from enjoying life and above all their fundamental rights and freedoms. It further prevents them from realizing their fullest potentials and possible contributions and benefiting equitably from development of their families and societies. In many ways violence against women retards their efforts for personal advancement and impedes efforts towards poverty reduction because women’s potential is not utilized optimally.

According to WHO -up to 70 per cent of women experience physical or sexual violence in their lifetime. Among women aged between 15 and 44, acts of violence cause more death and disability than cancer, malaria, traffic accidents and wars combined. In Sub-Saharan Africa, between 13 per cent and 45 per cent of women suffer assault by their intimate partners during their lifetime and as we speak over 3 million girls are at risk of female genital mutilation.

Ladies and Gentlemen;

Violence against women is undermining our efforts to achieve the Millennium Development Goals in Africa. We know for a fact that some African countries will not achieve the MDGs that have key indicators on gender matters and others partly because of gender based violence. The objective of reducing poverty, ending hunger, deprivation and promoting socio-economic development for all peoples on all continents will not be realized if violence against women and girls continues. The gender related MDG include MDG 2, on access to universal primary education; MDG 3 on promoting gender equality and empowering women and MDG 5 on reducing maternal mortality.

We cannot achieve our objectives if young girls are being abducted on their way to or from school. If in many of our countries, girls are forcefully married off at a very tender age, putting them at risk of getting pregnancy at too young an age and at risk of contracting HIV/AIDS and other sexually transmitted diseases. Shamefully there are over 14.1 million girls in Sub-Saharan Africa who are child brides, married before the age of 18.

Ladies and Gentlemen;

Violence against women and girls is a daily occurrence, it takes place during times of peace in the confines of homes, in the streets, in the bushes and everywhere. It is exacerbated during conflict where rape becomes a weapon of war. It affects women of all ages: children, teenagers, adults and elders. Nobody is spared. It is not uncommon these days to hear reports of elderly men have defiled girls under 10 years old, or young men being incarcerated for having abused elderly women who are their mothers or even grandmothers. This is not only an expression of moral decadence of the highest order happening in our societies, it is, also, cruel, inhumane and above all criminal. It therefore, deserves our unequivocal condemnation and calls for concerted efforts to end this diabolic behaviours and actions. We cannot swallow our pride.

Measures to Address Violence against Women

Ladies and Gentlemen;

I am pleased to note that while the situation may look challenging, but it’s not hopeless. African Heads of State and Government have taken a positive stand. Firstly, we enshrined in Article 4 (L) of the Constitutive Act of the African Union the inclusion of the gender parity principle. This provides for a moral obligation for all Member States to enshrine this principle in their national constitutions, legislations and socio-economic development policies and programmes.

I want to assure you that Tanzania remains committed to the pursuit of gender parity and fighting violence against women. We will not falter in this endeavour. I am ready to work with my colleagues in other countries to promote this noble cause in the African continent.

Secondly, we have the ground breaking Protocol on African Charter on Human and People’s Rights on the Rights of Women in Africa. The Protocol was adopted by the African Union on 11 July 2003 at its second summit in Maputo, Mozambique. On 25 November 2005, having been ratified by the required 15 Member States of the African Union, the Protocol entered into force. As of July 2010, a total of 28 Member States had ratified and deposited the instruments of ratification with the AU Commission. Today the Protocol is used as an important tool for holding Governments accountable on the commitments we have made.

Thirdly, we also have the Solemn Declaration on Gender Equality in Africa. As you know there are many other such instruments. In addition to these instruments, we also have various mechanisms that have been instituted to ensure that these frameworks are implemented. These are important frameworks that were adopted to facilitate actions to prevent and eliminate violence against women and girls and to provide for effective and adequate services to survivors.

Actions to address Gender based Violence

Ladies and Gentlemen;

We know that policies and legal instruments mean very little without commensurate implementation measures and actions. Governments have to walk the talk. We must ensure that our actions speak louder than words. It is required of us to adequately reflect on our national plans, programmes and budget measures to promote gender parity and fight against gender based violence.

The Africa UNiTE Campaign to End Violence against Women and Girls provides an important opportunity to galvanize us all into action to implement the frameworks and instruments I have referred to above. 

It provides us with an unprecedented opportunity to engage in innovative sustained actions to prevent, prosecute, punish and provide effective responses to violence against women and girls. It invigorates us to renew our commitments, to mobilize more strongly not only the Government entities but also the private sector, civil society, community based organizations, men and our traditional leadership structures and decision makers.

Indeed, the Campaign has placed the United Nations system at the center of such efforts. We look forward to engaging further with the United Nations in the country on how we can strengthen our national response. We want to ensure that we have a comprehensive response package to fighting gender based violence in the country. We want to report, in 2015, that indeed we have met the targets set out in the SADC Gender and Development Protocol. We look forward to both the technical and financial support to achieve this.

Conclusion

Ladies and Gentlemen;

I know most of you are now ready to start the climbing of Mt Kilimanjaro, therefore let me not delay you any further with a long speech. We wish you well and we hope that you will all reach the Uhuru Peak, the highest point of Mount Kilimanjaro and in Africa. With these remarks, I formally declare the Africa UNITE Climb to End Violence against Women and Girls officially launched.

Thank you for your attention and best of luck!

RAIS KIKWETE AWASILI MKOANI KILIMANJARO KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU

 Viongozi wa Kitaifa na wa Mkoa wa Kilimanjaro wakimsubiri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ashuke kwenye ndege katika uwanja wa Kilimanjaro International Airport tayari  kwa ziara ya kikazi ya siku tatu ya mkoa huo.

Miongoni mwa shughuli ambazo Mheshimiwa Rais atafanya ni pamoja na kuzindua kampeni ya kupinga ukatili na matumizi ya nguvu dhidi ya wanawake ambayo ataizindua kwa kuanzisha safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro iliyopewa jina la “Kilimanjaro Speak Out, Climb Up”.
Shughuli hiyo itakayofanyika kesho Jumatatu, Machi 5, 2012 asubuhi, imepangwa kwenye Lango la Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA)
Mbali na kuanzisha kampeni hiyo, Mhe Rais pia atafungua Mkutano wa Mwaka wa Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika kwenye Chuo cha Polisi mjini Moshi.
Hii ni ziara ya kwanza ya Mhe Rais Kikwete katika Mkoa wa Kilimanjaro tokea alipotembelea Mkoa huo wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi wa kada mbalimbali wa Kilimanjaro
 Rais Kikwete akiangalia burudani za ngoma
 Rais Kikwete akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh Leonidas Gama
 Rais Kikwete akisalimiana na wananchi wa Kilimanjaro waliofika kumlaki
 Rais akiendelea kusalimiana na wananchi wa kilimanjaro
 Kinamama wamejitokeza kwa wingi kumlaki
 Karibu Kilimanjaro….
 Ngoma za kiasili zikimtumbuiza wageni
 Msafara umewasili Ikulu ndogo ya Moshi, sasa ni utambulisho kabla ya breafing
 Kamati ya Ulinzi na Usalama
 Wakuu wa Wilaya za mkoa wa Kilimanjaro
 Viongozi wa taasisi mbalimbali katika kikao cha breafing
 Kikao kinaendelea
 Viongozi wa mkoa wa taasisi na idara mbalimbali
 Viongozi katika kikao hicho
 Wazee wa mji wa Moshi
 Wazee wa Moshi
 Kada mbalimbali za mkoa wa Kilimanjaro katika kikao hicho
 Mkuu wa Mkoa wa Kiliman jaro akitoa maelezo ya mkoa
 Kiongozi wa idara ya afya ya Mkoa akitoa maelezo yake 
 Taarifa ya elimu
 Taarifa ya hali ya mifugo
Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto Mh.Sophia Simba akitoa taarifa ya maandalizi ya kampeni ya kupinga ukatili na matumizi ya nguvu dhidi ya wanawake ambayo Rais Kikwete leo asubuhi ataizindua kwa kuanzisha safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro iliyopewa jina la “Kilimanjaro Speak Out, Climb Up”.

Rais Kikwete akutana na balozi wa Msumbiji nchini Mh. Amour Zacarias Kupela

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mh.Amour Zacarias Kupela wakati balozi huyo alipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo asubuhi na kufanya naye mazungumzo yanayohusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mh.Amour Zacarias Kupela baada ya balozi huyo kumtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo asubuhi na kufanya naye mazungumzo yanayohusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili.(picha na Freddy Maro)

Rais Kikwete apokea wadau wa kilimo ikulu Jijini Dar es Salaam leo

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na waziri wa Kilimo Profesa Jumanne Maghembe wakiwapokea wadau wa kilimo kutoka nchi mbalimbali za Afrika waliokwenda ikulu jijini Dar es Salaam kumpongeza kwa serkali yake kuanzisha mkakati wa Kilimo Kwanza nchini na kumuomba awasilishe ajenda ya kuboresha kilimo barani Afrika katika mkutano ujao wa wakuu wa nchi wa Umoja wa Afrika utakao fanyika nchini Malawi mwezi wa sita mwaka huu. Ujumbe huo ulikwenda ikulu kwa maandamano maalumu uliratibiwa na Shirika lisilo la kiserikali la ONE chini ya Mkurugenzi wake Dr.Sipho Moyo.(picha na Freddy Maro)

RAIS KIKWETE AOMBOLEZA KIFO CHA GEORGE FREDRICK MBOWE

Hayati George Fredrick Mbowe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Marehemu George Frederick Mbowe aliyefariki nyumbani kwake usiku wa kuamkia Jumatano tarehe 29 Februari, 2012 kutokana na ugonjwa wa Kiharusi.

Katika salamu zake hizo, Rais Kikwete amesema alimfahamu Marehemu George Mbowe enzi za uhai wake kama mchapakazi hodari aliyelitumikia Taifa lake kwa uzalendo, uaminifu na uadilifu mkubwa katika sehemu zote alizowahi kufanya kazi ikiwa ni pamoja na katika Utumishi wa Umma.

“Enzi za uhai wake, nilimfahamu Marehemu George Frederick Mbowe kama mtu aliyejituma kikamilifu katika utekelezaji wa majukumu yake na mchapakazi hodari”, amebainisha Rais Kikwete katika salamu zake.

 Amesema sifa hizo alizionyesha alipokuwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) na hata katika nyadhifa za Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Mwenyekiti wa PSRC na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Rais Kikwete ametoa pole nyingi kwa familia ya Marehemu George Mbowe kwa kuondokewa na mhimili muhimu wa familia, na amewahakikishia wanafamilia kwamba yuko pamoja nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa. Amewaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo ya mpendwa wao kwani yote ni mapenzi yake Mola.

Rais Kikwete amesema anamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipumzisha roho ya Marehemu George Frederick Mbowe mahali pema peponi, Amina.


01 Machi, 2012

HOTUBA YA RAIS KIKWETE KWA WANANCHI MWEZI FEBRUARI, 2012

Rais Kikwete akisoma hotuba yake ya mwezi wa Februari 2012 kwa Wananchi

Ndugu Wananchi,

Naomba sote tumshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma kwa kutuwezesha kuzungumza tena mwisho wa mwezi huu. Katika mwezi tunaoumaliza leo taifa letu lilipata msukosuko mkubwa kufuatia mgomo wa madaktari. Nashukuru mgomo huo umeisha lakini makovu yake yatabaki maisha katika kumbukumbu za historia ya taaluma ya tiba hapa nchini.

Leo, Mheshimiwa Waziri Mkuu amenipa taarifa kuwa Kamati aliyounda kushughulikia madai ya madaktari imekamilisha kazi yake na kuwasilisha taarifa yake kwake. Kuanzia kesho Serikali itaifanyia kazi taarifa hiyo na kuamua ipasavyo kulingana na uwezo uliopo. Nawaomba ndugu zetu madakatari kuwa na moyo wa subira.

 Napenda kutumia fursa hii kuwahakikishia ndugu zetu madaktari na watumishi wengine wote wa sekta ya afya kwamba Serikali inatambua, inajali na kuthamini kazi wazifanyazo na mchango wao katika kulinda na kudumisha afya za wananchi wa Tanzania. Aidha, narudia kutoa pole zangu za dhati kwa wananchi na hasa wagonjwa nchini kwa mateso waliyoyapata katika kipindi cha mgomo. Ni matumaini yangu kuwa hali kama ile haitajirudia tena katika nchi yetu.

Ndugu Wananchi.

Tukio lingine la kusikitisha ni mauaji ya Songea. Yapo yale yanayohusishwa na imani za ushirikina, na yapo yale ambayo yalitokea kwenye maandamano. Napenda kutumia nafasi hii kuelezea masikitiko yangu kwa vifo hivyo na kutoa pole na rambirambi zangu na za wananchi wa Tanzania kwa ndugu wa marehemu wetu hao. Tupo pamoja nanyi katika misiba hii mikubwa na majonzi.

 Napenda kuwahakikishia wananchi wa Songea kwamba Serikali kupitia vyombo vyake vya usalama imekuwa inafanya na itaendelea kufanya uchunguzi wa kina wa mauaji haya mpaka wahusika wote wapatikane na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Nimearifiwa kuwa, mpaka sasa kwa mauaji 13 yanayohusishwa na imani za ushirikina watuhumiwa 26 wamekwishakamatwa.

 Na kwa mauaji yaliyotokana na maandamano, askari polisi wanne wamekamatwa na upelelezi unaendelea.

Ndugu Wananchi;

Nashukuru kwamba amani na utulivu vimerejea katika Manispaa ya Songea. Nawapongeza sana viongozi wa ngazi zote na wananchi kwa ujumla kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuwezesha usalama na utulivu kupatikana. Tafadhali endeleeni na juhudi hizo mpaka mambo yatengemae kabisa.

Ndugu Wananchi;

Katika mwezi huu pia, Bunge letu Tukufu lilifanya mkutano wake wa sita na miongoni mwa maamuzi makubwa yaliyofanywa ni kupitisha Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 hususan kuhusu Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi kuhusu Katiba ya nchi. Nimekwishatia saini marekebisho hayo tarehe 20 Februari, 2012 na hivyo sasa yako tayari kutumika.

Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi kwa Wabunge wetu kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya ya kupitisha marekebisho hayo. 

 Aidha, natoa pongezi maalum kwa vyama vya siasa vya CCM, CHADEMA, CUF na NCCR – Mageuzi pamoja na Baraza la Taifa la Asasi Zisizokuwa za Kiserikali kwa maoni na mapendekezo yao ambayo ndiyo yalikuwa chachu ya marekebisho yaliyofanyika. Pia, nawashukuru kwa ushirikiano wao uliowezesha mafanikio kupatikana.

Tulipotoka

Ndugu Wananchi;

Bila ya shaka mtakumbuka kuwa baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Mabadikiko ya Katiba tarehe 18 Novemba, 2011, kulikuwepo na maneno mengi na maoni mbalimbali katika jamii. Wapo baadhi ya wadau hasa baadhi ya vyama vya siasa na asasi za kiraia ambao waliniomba nisitie sahihi Muswada huo kuwa Sheria na badala yake niagize Bunge liuzungumze upya. Aidha, vyama vya siasa vya CHADEMA, CUF na NCCR – Mageuzi na Baraza la Taifa la Asasi Zisizokuwa za Kiserikali waliomba kukutana nami tuzungumzie mchakato mzima wa Katiba. Sikusita kuwakubalia na kwa nyakati mbalimbali tulikutana na kuzungumza nao.

Ndugu Wananchi;

Katika mazungumzo yangu nao niliwaeleza ugumu niliouona kuhusu kuacha kutia sahihi Muswada huo na kuurudisha tena Bungeni kujadiliwa upya. Nilichelea kuliingiza taifa letu katika mgogoro mkubwa wa kisiasa na kikatiba usiokuwa na lazima. Mgogoro ambao tunaweza kuuepuka kwa kutumia njia nyingine za kikatiba na kisheria kufikia malengo yale yale. Kitendo cha mimi kukataa kutia sahihi kingejenga chuki kwa upande wa Wabunge walio wengi ambao waliujadili Muswada na kuupitisha. Wengeweza kuhisi wamedharauliwa na kuonekana hawana thamani.

Katika mazingira hayo mtakapowarudishia Muswada huo kuujadili kuna hatari ya kutokupata ushirikiano wao na kushindwa kupata kile kinachotarajiwa. Wanaweza kujadili na kuamua kukataa mapendekezo yote mapya na kubakia na msimamo wao ule ule.

Ndugu Wananchi;

Kwa ajili hiyo, busara ilinielekeza kuwa tusitumie njia hii bali tutumie njia za kawaida za kufanya marekebisho ya Sheria zilizotungwa na Bunge. Hakuna Sheria iliyotungwa na Bunge ambayo haiwezi kufanyiwa marekebisho. Kinachotakiwa ni kupeleka mapendekezo ya vifungu au vipengele vya Sheria husika vinavyotakiwa kurekebishwa.  Bunge litavijadili na kama hoja zinatosheleza vitafanyiwa marekebisho. Mimi nilipendelea busara na hekima hiyo. Niliwaeleza wadau sababu za kuamua kutia sahihihi Sheria na kuwasihi wakubali tufanye lililo bora zaidi ambalo ni kupeleka Bungeni mapendekezo ya sheria hiyo katika maeneo ambayo tunataka marekebisho hayo yafanywe.

Nilitahadharisha kuwa hata kufanya hivyo kunaweza kuwa na ugumu wake hasa pale dhana zisizokuwa sahihi zitakapopandikizwa kwa Wabunge. Niliwaomba tushirikiane kuhakikisha dhana potofu hazijitokezi na zinapojitokeza tuzisahihishe. Niliwahakikishia utayari wa Serikali kushirikiana nao katika hatua zote, tangu kutayarisha mpaka kuwasilisha mapendekezo hayo Bungeni iwapo watapenda Serikali ifanye hivyo. Aidha, niliwaambia kuwa hata sisi Serikalini tulikuwa na dhamira ya kupeleka marekebisho kwa baadhi ya vifungu vya Sheria hiyo kwa sababu mbalimbali.

Nafurahi kwamba, kwa pamoja licha ya tofauti zetu kuhusu uamuzi wangu wa kutia saini Muswada tulikubaliana kushirikiana kutoa mapendekezo ya marekebisho ya Sheria hiyo, ambayo tuliyawasilisha katika Bunge lililopita. Nafurahi na kufarijika kwamba, baada ya mjadala mkali, na Wabunge kufanya marekebisho kadhaa na hata kuingiza mambo mengine mapya, Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ulipitishwa na Bunge tarehe 10 Februari, 2012. Baadaye uliwasilishwa kwangu na nikatia sahihi kuwa Sheria tarehe 20 Februari, 2012. Sina budi pia kukitambua Chama cha Mapinduzi ambacho kilileta mapendekezo yake. Mapendekezo hayo yalizingatiwa kama ilivyofanywa kwa yale ya wadau wengine.

Ndugu Wananchi;

Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi maalum kwa vyama vya siasa vya CHADEMA, CUF, NCCR – Mageuzi na CCM na Baraza la Taifa la Asasi Zisizokuwa za Kiserikali kwa uelewa wao na ushirikiano wao kulikotuwezesha kufikia hapa tulipo katika mchakato wa kutengeneza Katiba Mpya kwa usalama, utulivu na kwa maelewano. Kwa kweli, jinsi hali ilivyokuwa huko nyuma, hatuna budi kushukuru na kujipongeza. Ni matumaini yangu na rai yangu kuwa tutaendeleza ushirikiano na utamaduni huu wa mazungumzo tuliouanzisha na kuutumia katika hatua zingine zinazofuata.

Nchi imetulia joto na jazba kuhusu Katiba havipo. Kumbe tukiamua na hasa tukizungumza inawezekana. Naomba wadau wote tuazimie kuwa mambo yaendelee hivi hata katika hatua zijazo za mchakato huu na masuala mengine muhimu kwa maslahi ya nchi yetu na watu wake.

Ndugu Wananchi;

Katika mazungumzo yetu na wadau tulikubaliana kwamba tushughulikie marekebisho ya Sheria hii kwa awamu. Kwa kuanzia tushughulikie mambo yanayohusu Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi Kuhusu Katiba ili iundwe na kuanza kazi. Baada ya hapo tuangalie mambo yahusuyo Bunge Maalum na Kura ya Maoni.

Bahati nzuri Sheria ya sasa inaelekeza kuwa Kura ya Maoni itatungiwa Sheria yake maalum, hivyo mambo yanaweza kusubiri wakati huo. Hivyo basi, baada ya muda si mrefu, Serikali na wadau tutaanza mazungumzo kuhusu mapendekezo ya marekebisho kuhusu Bunge Maalum. Kama yatakuwepo na kama kutafikiwa makubaliano, mapendekezo yatafikishwa katika Bunge letu tukufu kwa hatua zipasazo.

Ndugu Wananchi;

Bahati nzuri pia kuna kipindi kirefu kidogo wakati Tume inaendelea na kazi yake mpaka hapo Bunge Maalum litakapoanza kazi. Tume imepangiwa kukamilisha kazi yake ndani ya miezi 18 na inaweza kuongezwa miezi miwili. Wadau wanaweza kutumia sehemu ya muda huo wa Tume kushughulikia na kufanya marekebisho yahusuyo Bunge Maalum.  Hata hivyo, kama mapendekezo yatakamilika mapema ni bora zaidi yafikishwe Bungeni na kushughulikiwa ipasavyo.

Wadau Kupendekeza Majina

Ndugu Wananchi;

Miongoni mwa marekebisho muhimu yaliyofanywa katika Sheria ya Mabadiliko ya Katiba katika Bunge lililopita ni kuwekwa kwa utaratibu wa wadau kupendekeza kwa Rais majina ya watu wanaoona wanafaa kuteuliwa kuwa Wajumbe wa Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni kuhusu Katiba. Nafurahi kutoa taarifa kwamba nimekwishatoa mwaliko kwa wadau husika, yaani vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, jumuiya za kidini, asasi za kiraia pamoja na jumuiya, taasisi na makundi mengine yenye malengo yanayofanana kuleta mapendekezo hayo.

Mwaliko wangu huo umeshatangazwa katika Gazeti la Serikali Namba 66 la Ijumaa tarehe 24 Februari, 2012. Kuanzia kesho itatangazwa katika magazeti ya kawaida. Katika mwaliko huo, wadau wanatakiwa kupendekeza majina yasiyozidi matatu ya watu wanaokidhi sifa zilizotamkwa katika kifungu cha 6 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Sifa hizo ni hizi zifuatazo:-

(a) Uzoefu katika kufanya mapitio ya katiba na sifa za kitaaluma za wajumbe kwenye mambo ya katiba, sheria, utawala, uchumi, fedha na sayansi ya jamii.

(b) Jiografia na mtawanyiko wa watu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na

(c) Umri, jinsia na uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kijamii.

Aidha, nimeelekeza kuwa siku ya mwisho ya wadau kuwasilisha mapendekezo yao ni tarehe 16 Machi, 2012. Wadau wanatakiwa kupitishia mapendekezo yao kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Muungano au Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Nimewapa viongozi watendaji wakuu hao jukumu la kupokea mapendekezo ya majina na kuyawasilisha kwangu. Baada ya hapo nitashauriana na Rais wa Zanzibar kuteua Wajumbe wa Tume pamoja na Mwenyekiti na Makamu wake.

Ndugu Wananchi;

Sheria ya Mabadiliko ya Katiba pia inatoa fursa kwa Rais kuteua Wajumbe wa Tume kutoka hata nje ya orodha ya wadau. Ilionekana ni vyema kufanya hivyo kwani wapo watu wengine wazuri ambao wanaweza kuwa hawamo katika makundi yaliyotajwa na Sheria hii. Aidha, upo uwezekanao kwa mapendekezo ya makundi kutozingatia baadhi ya mambo ya msingi kama vile jinsia, jiografia na mtawanyiko wa watu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kadhalika. Fursa hii aliyopewa Rais itasaidia katika kuzingatia matakwa haya ya Sheria.

Pamoja na hayo napenda kuwahakikishia kuwa iwapo nitaitumia fursa hiyo watu hao hawatakuwa wengi kuliko wale waliopendekezwa na makundi yaliyotajwa katika kifungu cha 6 (6) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Ndugu Wananchi;

Napenda kutumia nafasi hii kuwakumbusha wadau na wananchi kwa jumla kuwa Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni Kuhusu Katiba ina Wajumbe 30 tu wanaopatikana kwa idadi sawa kutoka sehemu zotu mbili za Muungano wetu yaani 15 kutoka Tanzania Bara na 15 kutoka Zanzibar. Unapoongeza Mwenyekiti na Makamu wake kwa jumla Tume itakuwa na wajumbe 32 yaani 16 kila upande. Hivyo basi, fursa ya kila aliyeleta majina kupata nafasi katika Tume si kubwa.

Nayasema haya kutahadharisha juu ya ukweli huu ili tusijipe matumaini makubwa mno na wala tusije tukashutumiana baada ya uteuzi. Hata hivyo, pamoja na ugumu wa kuchagua miongoni mwa orodha ya watu wengi wazuri, nitajitahidi tu Wajumbe wa Tume wawe watu makini, wanaowakilisha sura pana ya jamii za nchi yetu na makundi yake muhimu na utashi wa watu wa Tanzania yetu.

Tunapokwenda

Ndugu Wananchi;

Ni matarajio yangu kuwa zoezi la kuunda Tume litakamilika muda mfupi kadri inavyowezekana, baada ya kupokea mapendekezo ya makundi. Kama nilivyokwishawahi kudokeza siku za nyuma, napenda Tume ikamilike kuundwa katika robo ya pili ya mwaka huu na kuanza kazi muda mfupi baada ya hapo.

Naomba nitumie nafasi hii kutoa wito maalum kwa wananchi wenzangu kuanza kujiweka tayari kutoa maoni yao kwenye Tume. Mambo yataanza miezi michache ijayo. Najua Tume itatengeneza utaratibu wa kuelimisha wananchi kuhusu Katiba. Lakini nawaomba kila mtu binafsi yake aanze kuchukua hatua za kuifahamu Katiba iliyopo sasa ili apate ufahamu wa maudhui muhimu ya Katiba. Kufanya hivyo kutamuwezesha kuamua kwa usahihi anataka kupendekeza nini kiwemo katika Katiba mpya. Nimeagiza Mpiga Chapa wa Serikali kuhakikisha kuwa vitabu vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vinachapishwa kwa wingi ili wananchi waweze kuwa navyo na kuvisoma. Inawezekana, Timiza Wajibu Wako.

Asanteni sana kwa kunisikiliza.

Mungu Ibariki Afrika!

Mungu Ibariki.

Mungu Ibariki Tanzania.

PHOTOS AND SPEECH BY PRESIDENT JAKAYA MRISHO KIKWETE AT THE LAUNCH OF THE PRESIDENTIAL AWARD ON THE EXTRACTIVE INDUSTRY CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITIES AND EMPOWERMENT (CSRE) HELD AT HYATT KILIMANJARO HOTEL ON 28th FEBRUARY

Hon. William Ngeleja, Minister for Energy and Minerals;

Hon. Ministers, Deputy Ministers,

Hon. Regional Commissioners;

Hon. Members of Parliament;

Ambassadors and High Commissioners;

Mr. Joseph Kahama, President of the Tanzania Chamber of Energy and Minerals;

Ms. Catherine Lyombe, Mining Stakeholders Forum;

Invited CEOs of Extractive Companies and Related Services; Representatives of Financial Institutions;

Distinguished Guests;

Ladies and Gentlemen;

I thank you honourable Minister for inviting me to participate at this historic event of launching the Presidential Award on the Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment Programme (CSRE). I am delighted that the Award will be contested annually and companies with outstanding performance will be acknowledged.

 

Ladies and Gentlemen;

I am happy with the key indicators developed to evaluate the scores for the Award.  In this regard, I consider very pertinent indeed, to include in the indicators things like;

  1. Community well-being and sustainability;
  2. Human resource development and training;
  3. Local industry participation;
  4. Community safety, water and environment;
  5. Social infrastructure such as housing and health services; and,
  6. Infrastructure development such as roads, electricity etc.

 

I commend you, and all those involved in conceiving the ideas and all those who made it happen as we are witnessing today.

The Presidential Award on CSR and Empowerment that we are launching tonight is an important milestone in the history of the extractive industry in Tanzania.  It is intended to align corporate policies and practices of companies in the extractive industry with sustainable development.  It is about making local communities where companies operate, benefit from the operations of the companies.    And, it is about the companies benefitting from the friendliness, harmony, understanding and cooperation that will ensue with the government and the people in the areas where the companies operate.

 

Business leaders;

Ladies and Gentlemen;

The concept of CSR is not new to Tanzania, the world and to all of us gathered here this evening.  Nowadays, it is increasingly becoming a normal international practice.  Almost all major companies in the country have put corporate social responsibility in their mission statements, policies and internal management systems.  What is new to us Tanzania, therefore, is the Award we are launching tonight.  Otherwise, companies have been working to ensure that local communities receive some direct benefits, and contribute to broadening social and economic sustainable development.

If principles of Corporate Social responsibility are observed and delivered, companies will enjoy very good relations with the communities around them.  If companies pay taxes that are due to the State, rightfully and timely, they will have good relations with the government.  Likewise, if the government and communities aptly deliver on their part of the responsibilities they will enjoy good relations with companies.  In the end everybody benefits and a win-win situation will be realised.  I believe, this is the best insurance policy one can long to have as an investor and as an investment destination.  If this is absent there is every risk of friction which is not healthy for business and may put the investment in jeopardy.  Everybody will be at risk losing.

Ladies and Gentlemen;

As alluded to earlier, under CSR and Empowerment, companies are expected to contribute to the provision of important social and economic services to the communities where companies are located.  Besides that, I would like to mention and underscore two or three importance things.  The first one is about sourcing goods and services locally.  Companies should make it their policy to engage local companies and local people in this regard.  There are services which can be sourced locally, there is no need of importing them from abroad.  This is the best way to promote local empowerment and an excellent way of promoting socio-economic growth in the economy of the area and the country.

This way, the company is integrating itself in the socio-economic life of the people by creating jobs and incomes.  It engenders, what economists call backward and forward linkages.  This will make the people strongly feel a sense of ownership and an obligation to protect the investment.  But if such things are absent people will have no stake in operations of the company.  As a result, they may care less about the presence, survival and progress of the company.  They may even turn hostile.  May I make a humble appeal to all companies in different sectors to take this matter seriously.

The other thing I would like to mention with regard to CSR policies is the relationship between large companies and small companies and local people engaged in the same industry.  It is incumbent upon large companies to realise that assisting local players to make progress is in their best interest.

Big companies should use their economic strength and technological capacity to help small players improve their operating systems, increase productivity, production and improve their affairs in general.  I believe, it will reduce jealousies, minimise friction, avoid unnecessary hostility and increase friendship and cooperation.  Take the case of artisanal mining activities in the vicinity of large mining operations in Tanzania.  If the latter assists the former and treat each other as partners, instead of competitors or contenders, it will very much improve relations between the two players who need each other.  It will clear undue misunderstanding and remove the mistrust and resentment.  Attitudes of hostility, threats and violence can easily be avoided.  In the end everybody benefits.

Ladies and Gentlemen;

The extractive industry can emulate the good practice of out-growers scheme around sugar plantations and sugar factories in Tanzania. In those cases, the large company supports small scale farmers, as out-growers, in several ways including provision of important services such as extension services, seedlings, technical know-how and market for their sugar cane.  I think this is a good model to look into.  It enhances local productive capacity and ensures sustainability of income to farmers. May this Award inspire companies in the extractive industry to emulate this example and strive to do what is possible to assist the local small scale investors grow and promote long-term economic and social sustainability.

Ladies and Gentlemen;

We in government consider CSR and Empowerment in the extractive industry very important indeed.  By their very nature, most of the operations in extractive industry are not renewable.  They get depleted as extraction continues.  As such if there are no proper arrangements for tangible benefits to the communities where the operations are located, they could easily become a source of discontent and resentment.  When the resources are completely exhausted and operations are stopped, the questions people would hasten to ask is about how did they benefit? The centrality of having mechanisms whereby communities and the country benefits even at the end of the life of the operations, therefore, need no emphasis.

We would like to see when such eventuality comes, everybody says we have benefited.  Contrary to that may create apprehensions and even resentment of large investors in the extractive industry especially when they are foreign based.  I believe, this is doable.    Let us heed the old adage “where there is will there is a way”.   Let us gunner the will to do it for our sake.

 

 

 

Honourable Minister;

Distinguished Guests;

Ladies and Gentlemen;

Before I conclude, let me, once again, sincerely thank the Mining Inter stakeholders’ Forum (MISF) and the Ministry of Energy and Minerals for conceiving the idea and introducing the CSRE Presidential Award in Tanzania. We are a little bit late, but it is better late than never.

I am confident the Award will stimulate and encourage the extractive companies to take interest in the communities around them and deliver on corporate social responsibility and empowerment. I invite business leaders here tonight to heed this our call and rise to the challenge.

With these many words, I now announce that the Corporate Social Responsibilities and Empowerment Presidential Award on Extractive Industry is officially launched.

 

Thank you for your kind attention!

 

 

 

Rais Kikwete Aagana na Mabalozi wapya wa Tanzania nchini Ubelgiji na Oman

Balozi mpya wa Tanzania nchini Ubelgiji Dr.Diodorus Kamala akiongea na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam wakati balozi huyo alipokwenda kumuaga leo asubuhi.

Balozi Mpya wa Tanzania nchini Oman,Mh.Ali Ahmed Saleh akiagana na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi kabla ya kuondoka nchini.(Picha na Freddy Maro).

Rais Kikwete arejea jijini dar leo

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Meck Said Meck Sadick wakati alipowasiri nchini leo akitokea nchini Botswana alikohudhuria Sherehe za Miaka 50 ya kuzaliwa kwa Chama Tawala cha nchi hiyo.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais-Mahusiano na Uratibu,Mh. Stephen Wassira wakati alipowasiri nchini leo akitokea nchini Botswana alikohudhuria Sherehe za Miaka 50 ya kuzaliwa kwa Chama Tawala cha nchi hiyo.Wengine Pichani ni Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard Membe (wa pili kushoto),Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaa,Suleiman Kova (kushoto).

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadick wakati alipowasiri nchini leo akitokea nchini Botswana alikohudhuria Sherehe za Miaka 50 ya kuzaliwa kwa Chama Tawala cha nchi hiyo.Wengine Pichani ni Viongozi Mbali mbali wa Serikali waliofika kumpokea Rais Kikwete leo.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Rais wa Botswana,Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama wakati alipokuwa akiondoka nchini Botswana mapema leo asubuhi,kurejea jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa Botswana wakati akindoka nchini humo kurejea jijini Dar es Salaam leo.Kushoto kwake ni Mwenyeji wake,Rais wa Botswana,Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama.

Rais Kikwete mgeni Rasmi katika sherehe za miaka 50 ya chama tawala cha nchini Botswana leo

Mgeni rasmi katika sherehe za miaka 50 ya chama tawala cha Botswana, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama wakiwa kwenye gari la wazi wakizunguka kuwasalimia wananchi waliofika kwa wingi katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Botswana leo kuadhimisha sherehe hiyo.

Mgeni rasmi katika sherehe za miaka 50 ya chama tawala cha Botswana, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama, Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Bw Kgalema Nontlanthe na Marais Wastaafu wa Botswana Sir Ketumile Masire ( wa pili shoto) na Bw Festus Mogae, wakijiandaa kukata keki ya sherehe hizo katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Botswana leo.

Mgeni rasmi katika sherehe za miaka 50 ya chama tawala cha Botswana, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama, Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Bw Kgalema Nontlanthe, na Marais Wastaafu wa Botswana Sir Ketumile Masire ( wa pili shoto) na Bw Festus Mogae, wakimwangalia Rais wa zamani wa Botswana akiwasha mwenge chini ya mti wa Marula palikoanzishwea BDP

Mgeni rasmi katika sherehe za miaka 50 ya chama tawala cha Botswana, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama, Makamuw a rais wa Afrika Kusini Bw Kgalema Nontlanthe, na Marais Wastaafu wa Botswana Sir Ketumile Masire ( wa pili shoto) na Bw Festus Mogae, wakiwa chini ya mti wa Marula ambako miaka 50 ilopita BDP ilizaliwa.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amekipongeza Chama Tawala cha Botswana, Botswana Democratic Party (BDP) kwa mafanikio yaliyopatikana nchini Botswana na watu wake.

Rais Kikwete ametoa pongezi hizo katika Sherehe za Kuadhimisha Miaka Hamsini (50) ya Chama cha BDP katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Botswana.

“Katika miaka hamsini ya uhai wake, BDP kimefanya mambo mengi mazuri nchini Botswana, katika ukanda huu na Afrika kwa ujumla na kimekuwa na historia nzuri ya kufanya mambo mengi mazuri ya kuvutia na kutolewa mfano barani kote” Rais amesema.

Rais Kikwete ametolea mfano wa Pato la ndani la Taifa la Botswana ambapo, wakati wa uhuru wa Botswana mwaka 1966, lilikuwa dola za kimarekani 70 tu, hadi kufikia dola za kimarekani 16,300 mwaka 2011.

“Haya ni mafanikio makubwa sana Barani Afrika” Rais amesema na kukipongeza kwa dhati Chama cha BDP ambacho kinatawala tangu uhuru wake.

Mapema akizungumza na wananchi Rais wa Botswana PM Gen. Seretse Khama Ian Khama ameeleza kuwa Tanzania imetoa mchango mkubwa na kuwa urafiki wa nchi mbili hizi ni wa kudumu.

“Tanzania imesimamia Uhuru, Haki na Ukweli barani Afrika” amesema na kueleza kuwa nchi yake itaendelea kusimamia na kuheshimu misingi hiyo.

Rais Khama pia amewakumbusha wanachama na wananchi wa Botswana kuwa umoja wao ndiyo ngao kubwa ya Chama cha BDP na kwamba chama hicho bado kiko imara kutokana na umoja wao huo na kinapania kuendeleza, kuuthamini na kuulinda Umoja wao.

Sherehe hizo zimehudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Bwana Wilson Mukama.

Rais Kikwete anatarajiwa kurejea Dar-es-Salaam kesho tarehe 26 Februari, 2012.

Mwisho.

Imetolewa na 

Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais,

Gaborone, Botswana

24 Februari, 2012

RAIS KIKWETE AWASILI GABORONE, BOTSWANA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama katika Uwanja wa Ndege wa Sir Serese Khama jijini Gaborone, Botswana,wakati Rais Kikwete alipowasiri nchini humo leo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo pia atahudhuria sherehe za miaka 50 tangu kuzaliwa kwa chama tawala cha nchini huko cha BOTSWANA DEMOCRATIC PARTY.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama wakati alipowasili Uwanja wa Ndege wa Sir Seretse Khama jijini Gaborone, Botswana, leo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo pia atahudhuria sherehe za miaka 50 tangu kuzaliwa kwa chama tawala cha nchini huko cha BOTSWANA DEMOCRATIC PARTY.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mwenyeji wake Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama wakiangalia ngoma mashuhuri ya makhirikhiri.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua paredi ya Majeshi ya nchi hiyo.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa kwa shangwe baada ya kuwsili Gaborone.

 

RAIS KIKWETE KATIKA MKUTANO WA KUJADILI SOMALIA JIJINI LONDON LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Lancaster House jijini London leo February 23, 2012 kijiunga na viongozi wa nchi mbalimbali katika mkutano wa kujadili mstakabali wa nchi ya Somalia ambayo imekuwa katika misukosuko kwa zaidi ya miaka 20 ambapo jumuiya ya kimatifa ikiongozwa na Uingereza imepania kumaliza matatizo mbalimbali katika nchi hiyo ikiwemo kutokuwa na serikali inayoeleweka, uharamia, ugaidi pamoja na kujaribu kurudisha amani.PICHA NA IKULU.

PRESIDENT KIKWETE MEETS UK’s Foreign Minister William Hague in London

President Jakaya Mrisho Kikwete chats  with UK’s  Secretary of State for Foreign and Commonwealth Affairs of the Mr William Hague (middle) and UK’s Parliamentary Under Secretary responsible for Africa, United Nations, economic issues, conflict resolution, and climate change Mr Henry Bellingham after their talks at the Foreign office  in London today February 22, 2012.  The UK will host a conference on Somalia tomorrow February 23, 2012 with the view to  pulling  together international effort to help Somalia to its feet after 20 years of sliding backwards, despite the efforts of the African Union, the United Nations and the international community, international policy towards the country.  
For full details on the Conference CLICK HERE

Rais Kikwete akabidhi kifuta machozi cha ng’ombe longido, azindua mradi wa uwezeshaji mifugo

Rais Dr.Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Longido wakati wa hafla ya kugawa ng’ombe zaidi ya 25,000 na mbuzi zaidi ya 15,000 kwa kaya zilizoathirika kwa ukame wilayani Longido jumapili.
Mwanafunzi Godlisten Ole Olais anayesoma kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya Longido akiteta jambo na Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili katika viwanja vya sekondari hiyo kuongoza uzinduzi wa wa mradi wa serikali wa uwezeshaji mifugo(seed stock) kwa kaya za wafugaji waliopoteza mifugo yote kutokana na ukame msimu wa 2008-2009 na 2009-2010 zilizofanyika wilayani longido jumapili.
Viongozi wa kabila la Kimasai(Laigwenani) wakimpa Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete zana za kijadi za uongozi mkuki na fimbo wakati wa hafla ya kukabidhi ng’ombe iliyofanyika wilayani Longido jumapili.
Mmoja wa Wazee wa Kimasai akimuombea dua Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wilayani Longido Jumapili.
Mzee wa Kimasai mkazi wa Longido akimshukuru na kumuombea dua njema Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete baada ya mzee huyo kukabidhiwa ng’ombe watano na mbuzi watano wilayani Longido jana.Mzee huyo ni mmoja wa wafugaji walipoteza mifugo yao yote kufuatia ukame mkali uliozikumba wilaya za Longido,Ngorongoro na Monduli.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mmoja wa wakazi wa Longido ngombe watano na mbuzi katika sherehe ambayo jumla ya kaya 16 zilikabidhiwa ngombe na mbuzi baadaya kuathirika na janga la kiangazi ambapo baadhi wakazi wa wilaya za Longido,Ngorongoro na Monduli walipoteza mifugo yao yote.Katika zoezi hilo serikali imetoa jumla ya ngombe zaidi ya 25,000 na zaidi ya mbuzi 15,000 ili kuzisaidia familia hizo kuanza tena maisha yao yanayotegemea sana mifugo.Sherehe za makabidhiano hayo zimefanyika wilayani Longido, mkoani Arusha. 

Morani wa kimasai wakicheza ngoma maalumu wakati wa sherehe hizo.Picha na  mdau Freddy maro wa Ikulu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mradi Kabambe wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo (Seed Stock) wa kutoa kifuta machozi cha mifugo kwa maelfu ya wananchi katika wilaya tatu za Mkoa wa Arusha mifugo ambao walipoteza mifugo yao wakati wa ukame mkubwa ulioendelea kwa miaka mitatu mfululizo katika wilaya hizo.

Rais Kikwete amezindua Mradi huo katika sherehe kubwa iliyofanyika mjini Longido leo, Jumapili, Februari 19, 2012, ambako amekabidhi ng’ombe jike watano na mbuzi watano kwa kila moja ya kaya 2,852 zilizopoteza mifugo hasa ng’ombe katika wilaya hiyo wakati wa ukame huo mkali ambao ulifikia kilele chake kwa mwaka 2008/2009.

Kiasi cha ng’ombe majike 500 wametolewa kwa wananchi wa Wilaya ya Longido katika sherehe ya leo iliyohudhuriwa na viongozi kutoka wilaya zote tatu wakiwemo viongozi wa Serikali, viongozi wa halmashauri, wabunge, viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa dini.

Katika sherehe hizo zilizohudhuriwa pia na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mheshimiwa William Lukuvi wananchi wa Wilaya ya Longido wamemshukuru kwa dhati Mheshimiwa Kikwete na Serikali yake kwa kubuni na kutekeleza Mradi huo wa aina yake ambao haujapata kubuniwa ama kutelekezwa na Serikali yoyote tokea Uhuru.

Chini ya Mradi huo ambao utagharimu kiasi cha sh bilioni 11.2, kaya 6, 127 katika wilaya za Longido, Ngorongoro na Monduli, zote za Mkoa wa Arusha, zitapewa kifuta machozi cha ng’ombe majike watano na dume mmoja (ama mbuzi badala ya dume kama walivyoamua wananchi wa Longido), ili kuwawezesha wananchi kuanza tena kujenga misingi ya mifugo yao ambayo ilipotea katika ukame mkubwa ambao ulifikia kilele chake mwaka 2009.

Mbali na kutoa kifuta machozi cha mifugo, Serikali imekuwa inatoa misaada ya chakula cha dharura kwa wananchi wa maeneo hayo tokea wakati wa ukame huo. Wilaya ya Longido pekee yake mara nane imepokea chakula cha dharura cha kiasi cha tani 11,000 katika kipindi hicho.

Kwa mujibu wa kikosikazi cha Serikali kilichofanya tathmini ya upotevu wa mifugo kutokana na ukame huo, Wilaya ya Longido ilipoteza ng’ombe 231,832, mbuzi 171,435 na kondoo 92,235, Wilaya ya Ngorongoro ilipoteza ngo’mbe 115, 422 na Wilaya ya Monduli ilipoteza ngo’mbe 56,585, mbuzi 39,766 na kondoo 28,883.

Hatua ya utoaji ngo’mbe kwa wananchi wa Wilaya la Longido ambao utafuatiwa na utoaji wa ngo’ombe kwa wananchi wa wilaya za Ngongoro na Monduli, ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Mheshimiwa Rais Kikwete alipotembelea Wilaya ya Longido Agosti 23, mwaka 2009, na kushtushwa na madhara yaliyokuwa yamesababishwa na ukame katika wilaya hiyo. 

Rais Kikwete alirudia ahadi yake hiyo wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 katika mikutano yake ya kampeni mjini Longido na katika eneo la Namanga.

Kwa mujibu wa Mradi huo, jumla ya ngo’ombe 25, 055 na wastani wa mbuzi 14, 260 (watano kwa kila kaya) watatolewa na Serikali ambako Halmashauri ya Wilaya ya Monduli itapata ngo’mbe 6,184, Halmashauri ya Wilaya ya Longido ng’ombe majike 11, 408 na wastani wa mbuzi 14, 260 wakati Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro itapata ngo’mbe 7, 463.

Akizungumza katika sherehe hizo, Rais Kikwete amesema kuwa ngo’mbe wanaotolewa kwa wananchi siyo fidia ya mifugo yao ambayo ilipotea wakati wa ukame bali ni kifuta machozi tu.

“Hatuna uwezo wa kuwafidia wananchi ngo’mbe wote waliopotea katika ukame ule. Lakini kama Serikali lazima tufanye jitihada za kuwawezesha wananchi wa Masai kurejea katika shughuli yao kuu yaani ufungaji kwa kutoa kifuta machozi tu kidogo. Bila ngo’mbe hakuna Mmasai.”